logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bonface Mwangi atoa maoni yake kwa nini anahisi Kindiki hafai kushikilia ofisini ya umma

Mwangi amesema kwamba wakenya wengi wametekwa nyara na wengine kuulliwa kwa njia zisizoeleweka chini ya utawala wake.

image
na Brandon Asiema

Habari28 October 2024 - 16:28

Muhtasari


  • Mwanaharakati huyo aliwachiliwa huru Jumatatu asubuhi baada ya kukesha katika kituo cha polisi cha Kamukunji.
  • Kulingana na mwanaharakati huyo, hatua ya rais Dkt. William Ruto kumpandisha hadhi Kithure Kindiki kuwa naibu wa rais wa taifa la Kenya ni kuzidisha uhuru wa kiongozi huyo na uasi wa sheria.

caption

Muda mchache baada ya kuachiliwa bila mashtaka, mwanaharakati wa haki za kibinadamu Boniface Mwangi amesema kuwa waziri wa maswala ya ndani Kithure Kindiki hafai kushikilia nafasi katika ofisi ya umma.


Kupitia mtandao wake wa X, Mwangi amesema  kwamba wakenya wengi wametekwa nyara na wengine kuulliwa kwa njia zisizoeleweka  chini ya utawala wake kama CS wa usalama.


Kulingana na mwanaharakati huyo, hatua ya rais Dkt. William Ruto kumpandisha hadhi Kithure Kindiki kuwa naibu wa rais wa taifa la Kenya ni kuzidisha uhuru wa kiongozi huyo na uasi wa sheria.


“Chini ya uongozi wake, wananchi wametekwa nyara na kuuwawa na kumekuwa na ongezeko la kushangaza la mauaji ya wanawake.” Aliandika Mwangi.


Vile vile, mwanaharakati huyo ameitaka serikali kuzifidia familia ambazo zilipoteza wapendwa wao waliouliwa na polisi katika maandamano ya mwezi Juni ya kupinga mswada wa fedha.


Mwanaharakati huyo aliwachiliwa huru Jumatatu asubuhi baada ya kukesha katika kituo cha polisi cha Kamukunji.


Mwangi alikuwa amekamatwa Jumapili asunuhi nyumbani kwake Courage Base katika eneo la Ukambani kwa madai ya kuchochea wananchi kuandaa maandamano katika hafla ya mbio za Standard Chartered  marathon zilizofanyika Jumapili jijini Nairobi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved