logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DCI Wathibitisha Akaunti Zao X Na Facebook Kudukuliwa Usiku Wa Jumapili

Udukuzi huu unajiri siku chache baada ya akaunti za X za mashirika ya habari KBC na K24 kudukuliwa pia.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari10 February 2025 - 09:34

Muhtasari


  • “Kumbuka: Kwa hivyo habari hiyo ni FEKI na sio kutoka kwa DCI. Uhoji wa kina katika shughuli za uhalifu umeanzishwa ili kuwaweka rumande wahusika,” walisema.
  • Udukuzi huu unajiri siku chache baada ya akaunti za X za mashirika ya habari KBC na K24 kudukuliwa pia.

Idara ya Upelelezi wa Jinai DCI yathibitisha kudukuliwa akaunti za X, FB


IDARA ya upelelezi wa jinai, DCI wamefichua kwamba kurasa zao kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na X zilidukuliwa japo kwa muda mchache usiku wa Jumapili, Februari 9.


Sasisho hilo lilichapishwa kwenye ukurasa huo wa X saa chache baada ya msururu wa machapisho ya kutiliwa shaka kwenye ukurasa huo.


Kwa mujibu wa sasisho hilo, wadukuzi walifanikiwa kuchukua uthibiti wa akaunti zao kwa muda mfupi na kuanza kuchapisha jumbe za utani.


Hata hivyo, DCI waliweka wazi kwamba walifanikiwa kuzirudisha akaunti zao mikononi mwao na kuweka wazi kuwa machapisho hayo hayakuwa kutoka kwa idara hiyo ya upelelezi.


“Kwa muda fulani jioni hii, tulipata mashambulizi ya mtandaoni kwenye mifumo ya kidijitali ya DCI (X na Facebook), lakini tangu wakati huo tumepata udhibiti kamili. Katika kipindi kifupi, wahalifu wa mtandao waliojaribu kuchukua akaunti walichapisha maelezo yaliyonaswa kwenye picha ya skrini iliyo hapa chini,” DCI walisema kupitia X.


Idara hiyo ambayo imekuwa chini ya ukosoaji mkali kutoka kwa sehemu ya Wakenya kutokana na msururu wa utekaji nyara iliarifu kwamba uchunguzi dhidi ya tukio hilo la udukuzi umeanzishwa.


“Kumbuka: Kwa hivyo habari hiyo ni FEKI na sio kutoka kwa DCI. Uhoji wa kina katika shughuli za uhalifu umeanzishwa ili kuwaweka rumande wahusika,” walisema.


Udukuzi huu unajiri siku chache baada ya akaunti za X za mashirika ya habari KBC na K24 kudukuliwa pia.


 


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved