logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanaume Wanaotahiri Duniani Ni Dhaifu Na Wachafu – MP wa Homa Bay

“Ulimwenguni kote, tohara inafanywa na takriban 10% ya wanaume wadogo, dhaifu na wachafu.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari04 March 2025 - 15:00

Muhtasari


  • “Ulimwenguni kote, tohara inafanywa na takriban 10% ya wanaume wadogo, dhaifu na wachafu.”
  •  “Tukomeshe aina zote za ukeketaji nchini Kenya na kuwaepusha vijana wetu na maovu haya ya kijamii,” alitoa wito.

Peter Kaluma

PETER Kaluma, mbunge wa Homa Bay Mjini ameendelea kutetea msimamo wake kuhusu suala la kupashwa tohara kwa watoto wa kiume.

Kwa siku mbili mfululizo sasa, mbunge huyo amekuwa akipigia debe desturi ya kupasha tohara wanaume kupigwa marufuku nchini Kenya.

Baada ya kuweka chapisho la kutaka tohara ya wanaume kupigwa marufuku akisema kwamba inafuata itikadi za kizamani kwenye Biblia wakati wa Abrahamu, Kaluma amerudi akisema kwamba tohara ya wanaume hufanywa na takribani asilimi 10 tu.

“Ulimwenguni kote, tohara inafanywa na takriban 10% ya wanaume wadogo, dhaifu na wachafu. Tukomeshe aina zote za ukeketaji nchini Kenya na kuwaepusha vijana wetu na maovu haya ya kijamii,” alitoa wito.

Ameibua madai mengine akisema kwamba visa vya wasichana kupata mimba za mapema vimejaa katika jamii ambazo zinafanya tohara kwa wanaume.

Alitoa changamoto kwa jamii hizo akihoji kwa nini wanapasha tohara watoto wao wa kike kisha kukimbia kuwatafuta wanawake kutoka jamii za wasiokeketwa kama kweli wanaamini tohara ni jambo la maana.

“Ukeketaji, mimba za utotoni na ndoa za utotoni zimeongezeka katika jamii nyingi zinazofanya ukeketaji (tohara). Kwa nini wanaume kutoka katika jamii zinazofanya ukeketaji wakakata sehemu za siri za mabinti zao kisha kuwakusanya wanawake kutoka katika jamii ambazo hazifanyi hivyo, kama ukeketaji ni mzuri!” Kaluma aliongeza.

Tweet ya Peter Kaluma kuhusu tohara ya wanaume

Awali, Kaluma alikuwa ametaka kutupiliwa mbali kwa desturi ya kupasha tohara wanaume, akisema kwamba katika jamii zote za wanyama, binadamu tu ndio wanatahiri, jambo ambalo aliliona si sawa.

‘Acha kutahiriwa. Tohara ni kukata wanaume. Punda hawatahiri. Wanyama wote hutahiriwa isipokuwa wanadamu wachache ambao wamedanganywa kwamba wao ni wajukuu wa Abrahamu, mtu aliyeishi jangwani bila maji!” alisema.

Hata hivyo, maoni yake yamepokea pingamizi kali kutoka kwa watumizi wa mitandao ya kijamii, wengi wakidai kwamba tohara humfanya mtu kuwa msafi kinyume na Kauli yake kwamba wanaume wachache wanaotahiri ni wachafu na wadhaifu.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved