
Rais William Ruto ameahidi kuilinda Huduma ya Polisi ya Kenya, huku akiwaonya waandamanaji dhidi ya kuwachokoza maafisa walioko kazini.
Rais William Ruto ameahidi kuilinda Huduma Ya Polisi Ya Kenya, huku akionya waandamanaji dhidi ya kuwachokoza maafisa walio kazini.
Rais alitoa kauli hiyo katika Ikulu ya Nairobi alipokutana na maafisa pamoja na wachezaji wa Kenya Police FC na Kenya Police Bullets, ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Soka ya Kenya na Ligi Kuu ya Wanawake ya Kenya mtawalia.
“Hongera kwa Kenya Police FC na Kenya Police Bullets kwa ushindi wa heshima katika Ligi Kuu ya FKF na Ligi Kuu ya Wanawake ya FKF.”
“Kwa kila afisa wa polisi, kuanzia konstebo hadi askari wa kawaida mtaani, ninawapa hakikisho kuwa serikali ya Kenya itawaunga mkono na kusimama nanyi mnapolinda taifa letu na kuhakikisha familia zetu ziko salama,” Rais Ruto ameahidi.
Ruto alitoa ahadi hiyo Jumanne, Juni 24, katika Ikulu ya Nairobi wakati wa kifungua kinywa na mabingwa wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF), Kenya Police FC. Haya yanajiri licha ya ukaguzi mkali dhidi ya maafisa wa polisi kuhusu madai ya ukatili wa polisi na mauaji ya kiholela.
Kiongozi wa Taifa alitambua mchango wa pilosi katika kuwalinda Wakenya, mali na taifa kwa ujumla.
“Bila amani na usalama, hatuna taifa. Watu wanaoweka maisha yao hatarini kuhakikisha familia zetu, mali zetu na taifa letu lipo salama na thabiti ni vyombo vyetu vya usalama,” alisisitiza.
Wakati uo huo, Ruto alilaani vitendo vya kudhalilisha, kutisha na kushusha hadhi ya vikosi vya usalama, akiongeza kuwa mamlaka hizo zinastahili kupata msaada wote kutoka kwa taifa.
Licha ya kuahidi msaada wake, Ruto alibainisha kuwa vyombo vya usalama vitaungwa mkono tu ikiwa vitatenda kazi kwa mujibu wa sheria.
“Serikali hii itasimama nao ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria na kuhakikisha kuwa taifa ni salama. Tuna miundombinu ya kutosha kuhakikisha hili linafanyika kwa kuzingatia sheria,” alisema.
Ahadi yake inajiri siku moja kabla ya maandamano yaliyopangwa kufanyika katika eneo la Biashara Kuu la Nairobi (CBD) na maeneo mengine nchini, kwa heshima ya vijana wa kizazi cha Gen Z waliopoteza maisha yao wakati wa maandamano ya kupinga Mswada wa Fedha mwaka jana.
Polisi wameahidi kuwalinda Wakenya watakaoandamana, huku wakiwaonya dhidi ya kushiriki katika vitendo vya vurugu na kuchokoza mamlaka.
Licha ya ahadi hiyo, ripoti zimeibuka zikionyesha kuwa polisi huenda wakachochea vurugu, jambo ambalo waangalizi wengi wamedai litaletwa na wahuni wanaofadhiliwa na serikali.
Wakati huo huo, ahadi ya Ruto inapingana na hali halisi ya sasa nchini, ambapo taifa linakumbwa na matukio mawili makuu ambapo maafisa wa polisi wanahusishwa moja kwa moja na tuhuma za ukatili wa polisi.
Ruto alisema polisi wa Kenya ni nguzo kuu ya michezo nchini — wakizalisha si tu wanasoka wenye vipaji, bali pia wanariadha na wachezaji wa voliboli waliobobea.
“Tunajivunia mchango wao katika michezo yetu, na muhimu zaidi, katika kulilinda taifa letu. Tutasimama na polisi wetu na kuwaunga mkono, kwa kuwa wao ndio chanzo cha uthabiti na maendeleo ya Kenya,” alisema.