logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waititu ahukumiwa miaka 12, mkewe mwaka 1 kwa hatia ya ulaji rushwa

Kesi hiyo ambayo imekua ikiendelea kusikilizwa kwa zaidi ya miaka mitanno kufikia sasa hatimae imeamuliwa.

image
na Japheth Nyongesa

Hivi Punde13 February 2025 - 16:00

Muhtasari


  • Kesi hiyo ambayo  imekuwa ikiendelea kusikilizwa kwa zaidi ya miaka mitano kufikia sasa hatimae imeamuliwa.
  • Mke wa Waititu kwa upande wake alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini  ya shilingi 500,000.

Aliyekuwa Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu na mkewe Susan Wangari wamehukumiwa kifungo cha miaka 12 na mwaka mmoja jela mtawalia  baada ya kupatikana na hatia ya ufisadi kuhusiana na zabuni ya barabara ya shilingi milioni 588.

Kesi hiyo ambayo  imekuwa ikiendelea kusikilizwa kwa zaidi ya miaka mitano kufikia sasa hatimae imeamuliwa.

Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Milimani ya ufisadi Thomas Nzioki  siku ya Alhamisi, Februari 13 alimhukumu Waititu kifungo cha miaka 12 jela au kulipa faini ya shilingi milioni 53.5.

Zabuni hiyo ya yenye thamani ya shilingi 588,198,328 iliyohusisha ukarabati wa barabara kadhaa katika kaunti ya Kiambu, Thika, Limuru, Gatundu Kaskazini, Juja na Ruiru ilitolewa na serikali ya kaunti mnamo Februari 2018 kwa kampuni ya Testimony Enterprises Ltd.

Aliyekuwa waziri wa Barabara Kaunti ya Kiambu Luka Mwangi Wahinya, na mfanyabiashara Charles Mbuthia Chege pamoja na mkewe Beth Wangechi pia walipatikana na hatia ya njama ya ufisadi ya kuilaghai serikali ya kaunti ya Kiambu mamilioni ya pesa.

Siku ya Jumatano, Jaji Nzioki alitoa hukumu hiyo ambayo ilihitimisha malumbano ya kisheria ya miaka mitano baina ya washukiwa na Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC).

Mkewe Waititu kwa upande wake alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela au faini ya shilingi 500,000.

Hakimu Nzioki akitoa hukumu hiyo alipuuzilia mbali tetesi za Waititu kwamba kesi hiyo ilichochewa kisiasa na utawala uliopita wa Jubilee kutokana na uhusiana wake na Rais William Ruto wakati huo akiwa naibu wa rais.

Badala yake, hakimu alithibitisha kuwa upande wa mashtaka uliwasilisha kesi ya kulazimisha, iliyoungwa mkono na mashahidi 32 na vipande 129 vya ushahidi wa maandishi, ambao ulithibitisha hatia ya mshtakiwa bila shaka yoyote.

Baada ya kutathmini kwa makini ushahidi uliowasilishwa na pande zote na kwa kuzingatia kwa makini maoni, nina uhakika zaidi ya shaka yoyote kwamba upande wa mashtaka umethibitisha mashtaka dhidi ya watuhumiwa," Nzioki alieleza baada ya kuamua kesi hiyo

Hakimu Nzioki alimpata Waititu  na hatia ya makosa manne kwa kutoa zabuni ya KSh588 milioni bila kufuata utaratibu.

"Baada ya kutathmini kwa makini ushahidi uliowasilishwa na pande zote na kwa kuzingatia kwa umakini maoni, nina uhakika zaidi kwamba upande wa mashtaka umethibitisha mashtaka dhidi ya watuhumiwa,  Nzioki alisisitiza.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved