logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanahabari Richard Quest wa CCN amuoa ndume mwenzake

Wawili hao walipeana posa mwaka 2019.

image
na Radio Jambo

Kimataifa14 October 2020 - 13:43

Muhtasari


• Wawili hao walipeana posa mwezi Mei mwaka 2019, baada ya mpenzi wake kukubadi posa ya mwanahabari huyo.

• Tulisema  ‘I Do’ mwishoni mwa wiki. Siku bora zaidi katika maisha yetu.

• 2018, Quest alikataa kuomba msamaha kwa kukosoa hatua ya kuwabagua watu wenye uhusiano wa jinsia moja nchini Kenya.

Mwanahabari wa CNN Richard Quest hatimaye amefunga pingu za maisha na mpenziwe wa kiume Chris Pepesterny. 

Mwandishi huyo tajika wa habari ya biashara alizamia mitandao ya kijamii akielezea furaha yake kwa kusema "I DO" kwa barafu yake ya roho ambaye ni mwanamume mwenzake Chris na kuposti picha maridadi akiwa naye.

Quest aliandika kwa ujumbe wake; "Tulisema  ‘I Do’ mwishoni mwa wiki. Siku bora zaidi katika maisha yetu."

Wapenzi hao wawili walilazimika kuahirisha harusi yao mwezi Machi mwaka huu lakini wakaahidi kufunga ndoa kabla ya mwaka huu kuisha. 

"Leo Chris na mimi tulikuwa tuoane mjini London. Lakini ilibidi tuahirishe. Ni hatua ya kusikitisha lakini ilibidi. Tutaoana baadaye mwaka huu katika hafla kubwa...," alisema wakati wakiahirisha harusi yao. 

Wawili hao walipeana posa mwezi Mei mwaka 2019, baada ya mpenzi wake kukubadi posa ya mwanahabari huyo.

Mtangazaji huyo wa makala ya 'Quest Means Business' alizuru Kenya Oktoba 2018 ambapo alifunguka kuhusu uhusiano wake wa kimapenzi.

Katika mahojiano kwenye radio Quest alisema kwamba hataomba msamaha kwa kukosoa hatua ya Kenya kuwabagua watu wenye uhusiano wa jinsia moja.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved