logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanafunzi aangukiwa na jiwe kichwani ka kufa akifanya adhabu ya mwalimu shuleni

"Mmoja aliyekuwa ndani aliangukiwa na jiwe kubwa likampasua kichwa, likampasua utumbo wote ukawa nje."

image
na Radio Jambo

Makala18 March 2023 - 12:29

Muhtasari


• Mwanafunzi huyo wa kike aliangukiwa na jiwe kubwa kwenda ndani ya shimo alimokuwa akichimba kama adhabu ya mwalimu mkuu.

•Jiwe hilo lilimuangukia kichwani na kumpasua kifua hadi utumbo ukatoka nje, kifo ambacho kilitajwa kama cha ukatili.

Mwanafunzi wa kike aangukiwa na jiwe kichwani akichimba shimo kama adhabu ya mwalimu mkuu

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mwanafunzi wa shule ya upili nchini Tanzania ameripotiwa kufariki baada ya kuangukiwa na jiwe kichwani.

Mwanafunzi huyo anasemekana kupatwa na mwalimu mkuu akizungumza Kiswahili badala ya Kiingereza na kukabidhiwa adhabu ya kuchimba vifusi katika sehemu iliyokuwa na mawe makubwa.

Akiwa shimoni kuchimba, jiwe moja liliporomoka na kumuangukia kichwani na kumuua papo hapo katika kile mashuhuda walisema ni kifo cha ukatili.

Jiwe hilo kubwa lililoporomoka pia liliwajeruhi wanafunzi sita huku mmoja wao akivunjika mguu wa kulia na kupelekwa hospitalini kwa matibabu.

Kulingana na mzazi mmoja aliyekuwa akilalama, wanafunzi katika shule za msingi nchini Tanzania huwa hawafunziw Kiingereza na huyo ndio mara ya kwanza alikuwa amejiunga kidato cha kwanza akitokea msingi.

“Mwalimu mkuu ni mwanamke na watoto walikutwa wanaongea Kiswahili wakapewa adhabu ya kuchimba kifusi. Mmoja aliyekuwa ndani aliangukiwa na jiwe kubwa likampasua kichwa, likampasua utumbo wote ukawa nje, amekufa pale pale kifo cha ukatili kabisa,” mzazi huyo alieleza kwa uchungu.

Inaarifiwa kwamba mwalimu huyo mkuu mtoa adhabu baada ya kutaarifiwa kuhusu kilichotokea, alikimbia kwa kutumia pikipiki huku akiacha kila kitu chake nyuma ikiwemo leso na vitabu.

Kamanda wa polisi alidhibitisha kisa hicho na kusema kwamba wanafunzi hao ni miongoni mwa 30 waliopewa adhabu hiyo kali na isiyofaa kwa watoto wadogo.

“Wanafunzi ambao walikuwa wameongea lugha ya Kiswahili katika mazingira ya shule. Watoto Zaidi ya 30 na adhabu yenyewe ilikuwa ni kuchimba kifusi ili kuchota mchanga wa kuziba mtaro wa kupitisha maji. Mwanafunzi wa kike ndiye alifariki,” kamanda wa polisi alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved