logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Papa hayuko katika "hali nzuri kiafya', Vatican inasema

Msemaji wa Vatican Matteo Bruni aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatatu kwamba Papa alikuwa katika hali nzuri.

image
na Davis Ojiambo

Kimataifa18 February 2025 - 08:34

Muhtasari


  • Papa mwenye asili ya Argentina ametumia karibu miaka 12 kama kiongozi wa Kanisa Katoliki la Roma.
  • Amekuwa akikabiliwa na matatizo kadhaa ya kiafya katika maisha yake yote, ikiwa ni pamoja na kuondolewa sehemu ya pafu lake akiwa na umri wa miaka 21.
  • Hadhira ya maombi ya kila wiki ya Papa - ambayo kawaida hufanyika kila Jumatano - imeahirishwa kwa wiki hii, taarifa hiyo iliongeza.

PAPA FRANCIS

Papa Francis anatibiwa kutokana na kwamba hayuko katika "hali nzuri kiafya" na atasilia hospitalini kadiri na kutakavyokuwa na ulazima wa kufanya hivyo, Vatican imesema.

Papa mwenye umri wa miaka 88 alilazwa katika Hospitali ya Gemelli huko Roma siku ya Ijumaa ili kupata matibabu na kufanyiwa vipimo vya matatizo ya kupumua.

Katika taarifa zilizotolewa siku ya Jumatatu, Vatikani ilisema Papa ana "maambukizi yanayosababishwa na mchanganyiko wa virusi, bakteria na vimelea" katika njia yake ya kupumua, ambayo yanahitaji matibabu mengine.

Kabla ya kulazwa wiki iliyopita, Papa alikuwa na dalili za ugonjwa wa kupumua kwa siku kadhaa na alikuwa amewakabidhi maafisa kusoma hotuba zilizoandaliwa kwenye hafla.

Msemaji wa Vatican Matteo Bruni aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatatu kwamba Papa alikuwa katika hali nzuri.

Taarifa fupi kuhusu hali yake ilisema: "Vipimo vyote vilivyofanywa hadi sasa vinaonyesha hali yake sio ya kuridhisha na itahitaji alazwe hospitalini kupata matibabu mwafaka."

Hadhira ya maombi ya kila wiki ya Papa - ambayo kawaida hufanyika kila Jumatano - imeahirishwa kwa wiki hii, taarifa hiyo iliongeza.

Taarifa zaidi kuhusu hali ya Papa itatolewa baadaye Jumatatu, Bw Bruni aliongeza.

Papa mwenye asili ya Argentina ametumia karibu miaka 12 kama kiongozi wa Kanisa Katoliki la Roma.

Mnamo mwezi Machi 2023, aliwahi kulazwa katika hospitali hiyo hiyo kwa siku tatu na kupata matibabu ya matatizo kupumua.

Mnamo Desemba mwaka huo huo, alilazimika kukatisha safari yake ya kwenda Falme za Kiarabu kwa mkutano wa kilele wa hali ya hewa wa COP28 kwa sababu ya ugonjwa mwingine.

Amekuwa akikabiliwa na matatizo kadhaa ya kiafya katika maisha yake yote, ikiwa ni pamoja na kuondolewa sehemu ya pafu lake akiwa na umri wa miaka 21.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved