logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sera za Trump zaichanganya Ulaya

Viongozi wa Ulaya walikumbwa na Taharuki kubwa na sera za uongozi wa Rais Trump wa Marekani baada ya wao kutoalikwa katika mkutano.

image
na Evans Omoto

Kimataifa18 February 2025 - 11:31

Muhtasari


  • Rais wa Marekani Donald Trump alisema Jumapili kuwa anapanga kukutana na rais wa Urusi Vladimir Putin ili wawe na majadiliano kuhusu taifa la Ukraine.
  • Mataifa hayo yalielezea kuwa utawala wa Trump haukukuwa na uhakika asilimia 100 kuhusu kile kinachopaswa kufanywa kuhusu taifa la Ukreini.

 

Rais  wa Ufaransa  Emmanuel Macro na rais wa Marekani Donald Trump

Viongozi wa Ulaya walikumbwa na Taharuki kubwa na sera za uongozi wa Rais Trump wa Marekani baada ya wao kutoalikwa katika mkutano wa  majadiliano na Urusi kuhusu mustakabali wa Ukraine.

Rais wa Marekani Donald Trump alisema Jumapili kuwa anapanga kukutana na rais wa Urusi Vladimir Putin ili wawe na majadiliano kuhusu taifa la Ukraine.

Jumatatu Waziri mkuu wa Uingereza Sir Keir Starmer alisema Uingereza iko tayari na ina hamu kubwa ya kutaka kutuma jeshi la ardhini,msemaji wa masuala ya kigeni wa nchi  ya Ujerumani alisema kuwa taifa hilo liko tayari kutuma vikosi vya usalama ndani ya mfumo wa Kimataifa.

Mataifa hayo yalielezea kuwa utawala wa Trump haukukuwa na uhakika asilimia 100 kuhusu kile kinachopaswa kufanywa kuhusu taifa la Ukreini.

Hii ni fursa finyu sana kwa Ulaya ikijaribu kumshawishi Trump ambaye ni mshirika mkubwa katika suala hili la Ukreini na Urusi.Ambapo Ulaya imekuwa ikisisitiza kuwa hakuna maamuzi yatakayotolewa bila taifa la Ukreini kushirikishwa moja kwa moja.

Mataifa hayo ya Ulaya yalishangwa na usemi wa Rais Trump kuwa asingeshirikisha baadhi ya mataifa ya wanachama wa usalama.Kwa muda sasa Ulaya imekuwa ikitegemea  kivuli cha usalama kilichotolewa na Marejkani tangu vita vya pili vya dunia.

Kulingana na Vigezo vya majadiliano ya Urusi na Marekani  kuhusu Ukreini na jinsi ambavyo rais Putin amekuwa akijihisi kuwa na nguvu kutokana na hayo kuna hofu ya Ulaya kuwa hilo linaweza kubadilisha ufanisi wa usalama wa bara lao.

Kwa muda mrefu Putin kihistoria huchukia upanuzi wa Nato kuelekea nchi za Mashariki,  kwa hivyo nchi ndogo Jirani na urusi kama Baltiki na Polandi zinahisi kuwa hatarini.

Nchi za ulaya zikijumuisha Ufaransa,Ujerumani  na Uingereza zinaazimia  kuwa na mkutano mjini parisi Ufaransa ili kujadili hatima ya Ukreini ila hofu  yao ni kuwa je, Marekani itawaunga mkono katika suala la kuleta amani na ujulivu katika nchi hiyo?.

Hii inatokana na wito wa Trump kuitisha mkutano na rais wa Urusi pasi kuyajumuisha mataifa mengine ya wanachama jambo ambalo linaibua  maswali mengi  kuhusu mkutano huo wa Marekani na Urusi.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved