logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mjamzito ashinda Sh15.2m Baada ya Bosi Kumfuta na Kumtumia Emoji ya ‘Jazz Hands’

Kufutwa kazi kwake kulikuja baada ya mama huyo mjamzito kuomba kufanya kazi kutoka nyumbani kwa sababu alihisi “kichefuchefu" kwa sababu ya ugonjwa wake wa kutapika kila asubuhi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Mahakama18 February 2025 - 10:14

Muhtasari


  • Bw Kabir alimtumia ujumbe ulioishia na "Natumai kukuona hivi karibuni, tumepata mengi ya kufanya nje ya kazi" ikifuatiwa na "tabasamu la mikono ya jazz".
  • Emoji hiyo ilionyesha uso wenye tabasamu huku viganja viwili vya mikono vikitazama nje na inasemekana kuonyesha hisia za msisimko na shauku.

Mfanyikazi ashinda kesi baada ya mwajiri kumfuta kazi na kumtumia emoji ya 'jazz hands'

MSHAURI wa masuala ya uwekezaji mjamzito ameshinda zaidi ya £93,000 [Ksh 15,228,089] kama fidia baada ya bosi wake kumfukuza kazi na kisha kumtumia ujumbe wenye emoji ya "mikono ya jazz".

Kwa mujibu wa jarida la Telegraph, Ammar Kabir alimfukuza kazi Paula Miluska kwa kumtumia ujumbe "usioeleweka kwa makusudi" wakati akiwa mgonjwa, akielezea jinsi biashara "ilivyokuwa inataabika" na kwamba ilihitaji kupata mtu ambaye anaweza "kuwa ofisini", mahakama ilisikika.

Kufutwa kazi kwake kulikuja baada ya mama huyo mjamzito kuomba kufanya kazi kutoka nyumbani kwa sababu alihisi “kichefuchefu" kwa sababu ya ugonjwa wake wa kutapika kila asubuhi.

Alipokuwa akiwasilisha habari za kuachishwa kazi kwake, Bw Kabir alimtumia ujumbe ulioishia na "Natumai kukuona hivi karibuni, tumepata mengi ya kufanya nje ya kazi" ikifuatiwa na "tabasamu la mikono ya jazz".

Emoji hiyo ilionyesha uso wenye tabasamu huku viganja viwili vya mikono vikitazama nje na inasemekana kuonyesha hisia za msisimko na shauku.

Bi Miluska alituzwa fidia baada ya hakimu kuhitimisha kuwa alifukuzwa kazi isivyo haki kutokana na ugonjwa wake wa ujauzito.

Mahakama ya uajiri ilisikia kwamba Bi Miluska alianza kufanya kazi katika kampuni ya Roman Property Group Limited, iliyoko Birmingham, mnamo Machi 2022.

Mnamo Oktoba mwaka huo, mshauri wa uwekezaji aligundua kwamba alikuwa akitarajia mtoto na mwezi uliofuata, "alianza kuona madhara ya ujauzito wake kwa namna ya ugonjwa wa asubuhi".

Jopo hilo lilisikia ujumbe ambao Bi Miluska alituma kwa meneja wake Bw Kabir alipohitaji kuondoka kazini mapema kwa sababu ya "kichefuchefu kilichoongezeka" aliokuwa nao wakati wa ujauzito.

Siku iliyofuata, alimtumia ujumbe uliosema: "Mkunga alikuwa akisema kwamba kwa sasa ikiwa naweza kufanya kazi nyumbani itakuwa bora kwani wiki mbili zijazo kawaida huwa kilele cha kichefuchefu cha ujauzito kutokana na homoni.

Hakimu wa masuala ya uajiri alisema hakukuwa na "SMS nyingine" kati ya wawili hao hadi Novemba 26, Bw Kabir alipomuuliza Bi Miluska jinsi anavyohisi.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved