logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Zimbabwe: Mwanahabari Akamatwa Na Polisi Kwa Kumhoji Mkosoaji Wa Rais

Waendesha mashtaka walisema mwanahabari huyo alichochea vurugu kupitia mahojiano yake na kuiomba mahakama kumzuilia kwa saa 72 ili kuruhusu uchunguzi zaidi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Mahakama27 February 2025 - 09:00

Muhtasari


  • Waendesha mashtaka walisema mwanahabari huyo alichochea vurugu kupitia mahojiano yake na kuiomba mahakama kumzuilia kwa saa 72 ili kuruhusu uchunguzi zaidi.
  • "Ikiwa mshtakiwa atapewa dhamana, ataingilia mashahidi," mwendesha mashtaka alisema.
  • Amnesty International ililaani kukamatwa kwa Mhlanga na kutaka kuachiliwa kwake mara moja na kufutwa kwa mashtaka yote bila masharti.

mwanamume akiwa kwenye pingu za polisi

MWANAHABARI mmoja nchini Zimbabwe amezuiliwa na vyombo vya dola baada ya kufanya mahojiano na mkosoaji mmoja wa rais wa taifa hilo ambaye alimtaka kujiuzulu kwa kushindwa kuwafanyia wananchi kazi.

Kwa mujibu wa majarida kutoka Harare, Blessed Mhlanga, mwanahabari maarufu wa kituo cha Televisheni cha mitandaoni, Heart and Soul (HStv), amekuwa kizuizini tangu Februari 24 alipokamtwa.

Polisi walianzisha msako wa nchi nzima kumtafuta Mhlanga kufuatia mahojiano yake na Blessed Geza, kigogo wa chama tawala cha Zanu-PF na pia mkosoaji wa chama hicho, Januari 27 na Februari 11.

Geza, mkongwe wa vita vya ukombozi wa nchi hiyo vilivyopelekea uhuru mwaka 1980, alisema katika mahojiano hayo kwamba rais Emmeson Mnangagwa anapaswa kujiuzulu.

Pia alilaani mrengo wa Zanu-PF ambao umeripotiwa kupigia debe mipango ya kubadilisha katiba ili kumruhusu Mnangagwa, 82, kugombea muhula wa tatu.

Baada ya mahojiano hayo yenye ukakasi mwingi, kigogo huyo wa vita vya ukombozi wa Zimbabwe alichimba mitini na polisi walisema bado wanamsaka kwa udi na uvumba.

Waendesha mashtaka walisema mwanahabari huyo alichochea vurugu kupitia mahojiano yake na kuiomba mahakama kumzuilia kwa saa 72 ili kuruhusu uchunguzi zaidi.

"Ikiwa mshtakiwa atapewa dhamana, ataingilia mashahidi," mwendesha mashtaka alisema.

Amnesty International ililaani kukamatwa kwa Mhlanga na kutaka kuachiliwa kwake mara moja na kufutwa kwa mashtaka yote bila masharti.

"Uandishi wa habari sio uhalifu, na watendaji wa vyombo vya habari wanapaswa kufanya kazi zao bila hofu ya kulipizwa kisasi," shirika la kimataifa la haki za binadamu lilisema katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii.

Jukwaa la Kitaifa la Wahariri wa Zimbabwe lilisema "limefadhaishwa na kuhuzunishwa sana" na kukamatwa kwake, ambayo ni sawa na unyanyasaji wa mwandishi wa habari anayefanya kazi yake "kwa maslahi ya umma".

Zimbabwe imeorodheshwa katika nafasi ya 116 kati ya nchi 180 katika Maripota Wasio na Mipaka (RSF) 2024 World Press Freedom Index.

Vyombo vya habari "vimekabiliwa na mateso zaidi" tangu Mnangagwa kuchaguliwa tena kwa muhula wa pili mwaka 2023, kulingana na RSF yenye makao yake Paris.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved