logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wa Iria akashifu kutawazwa kwa Justin Muturi

Gavana wa Murang'a alisema kanuni za hekalu ya Mukurwe wa Nyagathanga zilikiukwa na sharti ibada ya kuitakasa ifanyike

image
na Radio Jambo

Yanayojiri23 May 2021 - 08:19

Muhtasari


•Gavana wa Murang'a alisema kanuni za hekalu ya Mukurwe wa Nyagathanga zilikiukwa na sharti ibada ya kuitakasa ifanyike

•Mwangi alisema kuwa jamii ya GEMA inalazimishwa kumpokea kiongozi ambaye hawajamteua

Murang.a.governor.Mwangi.wa.Iria.addresing.journalists.on.Wednesday

Spika wa bunge la kitaifa, Justin Muturi ametangaza kuwa yuko tayari kufikia viongozi wengine wa eneo la Mt Kenya na kujadiliana namna ya kuhakikisha kuwa maslahi ya eneo hilo yametimizwa.

Muturi amewapongeza wazee na viongozi walioshirikiana kuhakikisha kuwa ametawazwa kuwa msemaji wa GEMA na kusema kuwa ako tayari kuongoza.

“Nimenyenyekea sana kwa jukumu nililopewa la kuwa msemaji wa eneo la Mt Kenya. Nawashukuru wazeee wote na viongozi ambao wameshirikiana kuona kwamba jambo hili limefanikiwa na kwa kuniaminia kueleza ajenda za eneo hili” Muturi aliandika katika ukurasa wake wa Twitter.

Hafla ya kumtawaza Muturi ilifanyika katika hekalu ya Mukurwe wa Nyagathanga.

Hata hivyo, uteuzi wake kuwa sauti ya eneo hilo umeendelea kusutwa sana na baadhi ya viongozi kutoka eneo hilo ikwemo gavana Mwangi wa Iria wa kaunti ya Muranga.

“Nasikitika sana kwa niaba ya jamii yangu ya Wakikuyu kwa sababu hafla iliyokuwa na ugomvi mwingi na wazee kukosana ilifanyika huku imesimamiwa na polisi. Sisi tumekataa, Mungu wa Gikuyu hawezi tishiwa na bunduki. Tunataka mahala pale patakaswe na nimeomba wazee waniruhusu tuongozee hafla ya kutakasa hekalu ya Mukurwe ili tusije tukapata shida” Mwangi alisema.

Mwangi alisema kuwa jamii ya GEMA inalazimishwa kumpokea kiongozi ambaye hawajamteua. Alisisitiza kuwa kiongozi wanaomtambua ni rais Uhuru Kenyatta.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved