logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Joe Biden ateua balozi mpya wa Kenya

Alimuunga mkono Hillary Clinton wa Democrat katika kinyang'anyiro cha 2016 dhidi ya Donald Trump.

image
na Radio Jambo

Burudani09 December 2021 - 06:39

Muhtasari


• Rais wa Marekani Joe Biden amemteua aliyekuwa Afisa mkuu mtendaji wa kampuni ya Hewlett Packard (HP) na rais Meg Whitman kuwa balozi wa Marekani nchini Kenya. 

• Aligombea ugavana wa jimbo la California mwaka wa 2010 kwa chama cha Republican lakini akashindwa na mgombea wa Democrat Jerry Brown. 

• Alimuunga mkono seneta wa sasa Mitt Romney akigombea urais mwaka wa 2008.

Rais wa Marekani Joe Biden amemteua aliyekuwa Afisa mkuu mtendaji wa kampuni ya Hewlett Packard (HP) na rais Meg Whitman kuwa balozi wa Marekani nchini Kenya. 

Anatarajiwa kuchukua nafasi ya balozi Kyle McCarter aliyeondoka Januari 2021. Margaret C. Whitman (Meg), mkurugenzi mkuu wa biashara na mgombea wa zamani wa Gavana wa California, ni Mjumbe wa Bodi ya Procter and Gamble na General Motors, na Mwenyekiti wa Bodi ya Kitaifa katika shirika la Teach for America, Ikulu ya White House ilisema katika ujumbe wake. 

Whitman alitumia miongo kadhaa katika majukumu ya kiwango cha juu katika mashirika mbali mbali, lakini pia amekuwa katika siasa kwa miaka mingi. 

Aligombea ugavana wa jimbo la California mwaka wa 2010 kwa chama cha Republican lakini akashindwa na mgombea wa Democrat Jerry Brown. 

Alimuunga mkono seneta wa sasa Mitt Romney akigombea urais mwaka wa 2008 - kabla ya hatimaye kuwa mwenyekiti mwenza wa kampeni ya kitaifa ya Seneta John McCain mwaka wa 2012.  

Alimuunga mkono Hillary Clinton wa Democrat katika kinyang'anyiro cha 2016 dhidi ya Donald Trump.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved