logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ruto apongeza hatua ya Trump ya kubainisha jinsia mbili pekee, kiume na kike

Ruto amesisitiza haja ya kukumbatia sera ya wanawake na wanaume pekee.

image
na JAMES MBAKAjournalist

Yanayojiri26 January 2025 - 15:30

Muhtasari


  • Rais alisema anafurahi kwamba demokrasia kuu zaidi duniani imechukua hatua kutoa ufafanuzi juu ya suala ambalo limezua utata hapo awali.
  • Wiki iliyopita Rais Trump alitia saini amri za utendaji zinazothibitisha kwamba Marekani itatambua jinsia mbili pekee



Rais William Ruto mnamo Jumapili alikaribisha sera rasmi ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kutambua tu jinsia ya kiume na ya kike.

Rais alisema anafurahi kwamba demokrasia kuu zaidi duniani imechukua hatua haraka kutoa ufafanuzi juu ya suala ambalo limezua utata hapo awali.

“Kinyume na siku za nyuma, Marekani imekaribisha maendeleo fulani ambayo yanasisitiza mwelekeo wa kisera ulio wazi; wavulana wabaki kuwa wavulana, wanaume wabaki wanaume, wasichana wabaki wasichana, na wanawake wabaki wanawake,’’ Ruto alisema.

 Akiongea wakati wa ibada ya Jumapili katika kanisa kuu la The Global Cathedral jijini Nairobi, Ruto alisisitiza haja ya kukumbatia sera ya wanawake na wanaume pekee.

"Tumepata kuelewa kwamba mwelekeo wa sera za Marekani unaunga mkono kile tunachoamini," Rais Ruto alisema.

“Tunamshukuru Mungu kwamba mwaka huu, habari za kwanza kabisa kutoka Marekani katika utawala mpya ni kuthibitisha yale ambayo Biblia inasema, imani yetu inaamini nini na mapokeo yetu yanategemea msingi gani.’’

Wiki iliyopita Rais Trump alitia saini amri za utendaji zinazothibitisha kwamba Marekani itatambua jinsia mbili pekee, wanaume na wanawake, ambazo hazibadiliki.

"Tutaunda jamii isiyozingatia rangi na inayozingatia sifa. Kuanzia leo, itakuwa sera rasmi ya serikali ya Marekani kwamba kuna jinsia mbili pekee, wanaume na wanawake," Trump alisema katika hotuba yake ya kuapishwa.

Rais Trump aliamuru Jumatatu iliyopita alipokuwa akitaka kukomesha haraka sera mbalimbali zinazolenga kukuza usawa wa rangi na kulinda haki za watu wa LGBTQ+.

Agizo hilo linaitaka serikali kutumia neno "sex" badala ya "jinsia".

Pia inahitaji hati za utambulisho zinazotolewa na serikali, ikiwa ni pamoja na pasipoti na visa, ziwe kulingana na kile ilichoeleza kama "uainishaji wa kibayolojia usiobadilika wa mtu kama mwanamume au mwanamke."


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved