logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wetangula apuuza agizo la mahakama na kutangaza Kenya Kwanza upande wa Wengi

Spika Wetangula alieleza kuwa Mahakama haikutoa mwelekeo kuhusu ni upande upi ni wa wengi au walio wachache.

image
na Davis Ojiambo

Yanayojiri12 February 2025 - 17:26

Muhtasari


  • Katika uamuzi uliotolewa katika Bunge la Kitaifa siku ya Jumatano, Spika Wetangula alieleza kuwa Mahakama haikutoa mwelekeo kuhusu ni upande upi ni wa wengi au walio wachache.

Spika wa Bunge la Kitaifa Moses Wetang’ula akizungumza mnamo Januari 28, 2025
Spika wa Bunge la Kitaifa Moses Wetangula ametangaza Kenya Kwanza kuwa upande wa Wengi licha ya uamuzi wa mahakama ulioondoa hadhi ya chama tawala.

Katika uamuzi uliotolewa katika Bunge la Kitaifa siku ya Jumatano, Spika Wetangula alieleza kuwa Mahakama haikutoa mwelekeo kuhusu ni upande upi ni wa wengi au walio wachache.

Alibainisha kuwa hali ilivyo bado haijabadilika kwani Kenya Kwanza inajumuisha wabunge 165 huku Azimio ikiwa na wabunge 154. Katika orodha hiyo Wetangula alipokonya Azimio wabunge katika vyama tanzu ambao walitangaza kuhama muungano huo.

Zaidi ya hayo, Wetangula aliagiza kukatwa kwa rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu.

Uamuzi huo wa spika hata hivyo ulipingwa vikali na wabunge wa Azimio wakiongozwa na aliyeibua hoja hiyo Mbunge wa Suba Kaskazini Millie Odhiambo.

"Kama Azimio kwa heshima kubwa hatukubaliani na mawasiliano yenu na kama Azimio tutachukua hatua zaidi," Odhiambo alisema.

Baada ya uamuzi huo kutolewa kwa gadhabu Wabunge wa Azimio walitoka nje ya Bunge.

Majaji John Chigiti, Lawrence Mugambi, na Jairus Ngaah wiki iliyopita walikosoa msimamo wa Spika Wetangula kwa kukinzana na Msajili wa Vyama vya Kisiasa ambaye stakabadhi zake zilionyesha kuwa Azimio ilikuwa na wabunge wengi kufuatia matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2022 kabla ya wabunge 14 kugura na kujiunga na kujiunga na muungano tawala.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved