logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Spika Wetang'ula kwenye mizani ya sheria kisa uamuzi wa korti kuhusu waliowengi bungeni

Spika wa bunge la kitaifa Moses Masika Wetang'ula alikabiliwa na hali tete kisheria kufuatia uamuzi wake wa kutotii agizo la mahakama.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri24 February 2025 - 16:55

Muhtasari


  • Kutokana na tangazo lililotolewa mnamo Februari 12,2025 mahakama ilitoa uamuzi na kusema kuwa muungano wa Azimio ulikuwa na idadi kubwa ya wabunge kushinda muungano wa Kenya Kwanza.

Spika wa bunge la taifa Moses Masika Wetang'ula alikabiliwa na hali tete kisheria kufuatia uamuzi wake wa kutotii agizo la mahakama.

Kutokana na tangazo lililotolewa mnamo Februari 12,2025 mahakama ilitoa uamuzi na kusema kuwa muungano wa Azimio ulikuwa na idadi kubwa ya wabunge kushinda muungano wa Kenya Kwanza.

Mahakama ilitoa agizo hilo ikisesema kuwa ni kinyume cha Spika Wetang'ula kushikilia wadhifa huo kama spika wa bunge la taifa akiwa pia ndiye kiongozi wa Chama cha Ford Kenya wakati ambapo yeye pia ni mwanachama wa muungano wa kenya kwanza na vilevile mwanachama wa baraza la muungano wa Kenya kwanza.

Kutokana na hayo yote korti ilibaini kuwa ulikuwa ni ubatili na kinyume cha sheria hivyo ikatoa uamuzi wa spika kufanya mabadiliko ya kisheria na kuzingatia Katiba.

Wakati ambapo vikao vilirejelewa bungeni baada ya likizo fupi  spika aligairi kuzingatia maagizo ya mahakama na kuutangaza muungano wa Kenya kwanza kuwa ndio uliokuwa na idadi kubwa ya wabunge .

Kutokana na hilo la spika kutotii maamuzi ya mahakama walalamishi zaidi ya 12 walifika katika mahakama ya rufaa wakitaka mahakama hiyo kumshurutisha spika kutiii agizo la mahakama kuu na kuzingatia uamuzi uliotolewa na jopo la majaji watatu.

Walalalmishi hao wakiongozwa na Kennedy njagi,Suba chachi na Amos Wanjala walifika katika mahakama hio ya rufaa wakiwa na ombi la kurai mahakama iweze kubatilisha tangazo jipya la Spika la kutangaza tena muungano wa Kenya Kwanza kama waliowengi.

Kesi hio inajiri wakati ambapo mageuzi mbalimbali yanatarajiwa kufanywa katika kamati mbalimbali za mabunge yote mawili bunge la taifa na lile la seneti

Kulingana na maaumuzi ya spika Wetang'ula alisema kuwa katika maamuzi ya mahakama haikutoa maelezo zaidi ya ni nini kifanyike hivyo kuliacha bunge la taifa katika hali ngumu ya kutekeleza maamuzi hayo hivyo kusema kuwa maamuzi yote yalitolewa na bunge la taifa kwa sababu ni taasisi huru hivyo ilitekeleza  maamuzi yake pasi kuingiliwa wala kuegemea upande wowowte.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved