logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KPLC yatangaza maeneo yatakayoathirika na kukatizwa kwa umeme leo, Jumatatu

Kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyika kwenye mitambo.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri14 April 2025 - 07:43

Muhtasari


  • KPLC imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumatatu, Aprili 14.
  • Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Kakamega, Trans Nzoia, Meru.

Kenya Power

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumatatu, Aprili 14.

Katika taarifa ya Jumapili jioni, kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyika kwenye mitambo.

Walisema baadhi ya maeneo ya kaunti saba za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Kakamega, Trans Nzoia, Meru.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu za eneo la Galleria Mall zitaathirika na kukatizwa na umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Makutano na Ivona katika kaunti ya Kakamega yataathirika kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za maeneo ya Kapsara, Ngonyek, na Sibanga katika kaunti ya Trans Nzoia zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Meru, sehemu za maeneo ya Rubiri Kaubau na Kagwampugu zitakosa umeme kati ya saa mbili unusu na saa kumi na moja jioni.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved