logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto aonya wanasiasa na na vyombo vya habari dhidi ya kuingiza jeshi katika masuala ya kisiasa

Rais Ruto Jumatano ya tarehe 16 Aprili, 2025 aliwarai viongozi, wanasiasa kutoingiza siasa katika masual ya jeshi

image
na Evans Omoto

Yanayojiri16 April 2025 - 16:41

Muhtasari


  • Kiongozi wa taifa alisema hayo akirejelea matukio ya hapo awali ambapo viongozi wa kisiasa pamoja na vyombo vya habari viliweza kuchapisha habari kuhusu  jeshi la nchi.

President William Ruto presides over the Cadet Commissioning Parade in Lanet, Nakuru on April 16, 2025/PCS

Rais Ruto Jumatano ya tarehe 16 Aprili, 2025 aliwarai viongozi, wanasiasa kutoingiza siasa katika masual ya  jeshi

Rais Ruto alikuwa akizungumzia hayo alipokuwa Lanet akizindua hospitali ya ukanda huo wa Nakuru. Rais alizungumzia suala la jeshi la ulinzi la taifa  akisema kuwa hatakubali viongozi, wanasiasa au vyombo vya  habari kuweza kuliingiza  jeshi katika masuala ya siasa.

Kiongozi wa taifa alisema hayo akirejelea matukio ya hapo awali ambapo viongozi wa kisiasa pamoja na vyombo vya habari viliweza kuchapisha habari kuhusu jeshi la nchi. Hio ilifuatia kuwa kulikuwa na mkengeuko wa kizazi cha sasa cha GEN Z ambapo mara kwa mara wamekuwa

Kiongozi wa taifa alisema hayo akirejelea matukio ya hapo awali ambapo viongozi wa kisiasa pamoja na vyombo vya habari viliweza kuchapisha habari kuhusu  jeshi la nchi.

Hio ilifuatia kuwa kulikuwa  na mkengeuko wa kizazi cha sasa cha GEN Z ambapo mara kwa mara wamekuwa

wakimshutumu kwa kusema kuwa  ni lazima  aende alimaarufu ''Ruto must Go'' Jambo ambalo lilichochea usimamizi na viongozi wa ngazi za  juu za usalama kutoa kauli zao.

 Kiongozi wa kitengo  cha ujasusi  Nurdin Haji na Mwenzake  mkuu wa majeshi Charles Kahariri waliweza kuonya umma dhidi ya kutumia uhuru wao  wa mitandao kuweza kulitumbikiza  taifa katika hali ya mapinduzi au  kuharibu taifa   kwa masuala ya kibinafsi.

Ni kutokana  na matukio hayo  ambapo rais alitoa onyo kuhusu kuliingiza jeshi kwenye masuala ya siasa.

'' Kwa maendeleo ya kitaifa  hujengwa  kwa  misingi ya amani  uongozi mwema na ujumuishaji wa kila mmoja katika ufanikishaji wa maendeleo ya taifa. "

 "Vikosi vyetu  vya   usalama wa jeshi viko  imara kwa kuhakikisha kuwa vinatimiza haya  malengo na matakwa kwa hivyo  kuwepo kwao ni kujihakikishia kuwa   kunakuwa na usimamizi imara  ambapo husaidia  kuwavutia wawekezaji na huchochea   uhusiano  mzuri  wa nchi na wa kimataifa."

"Kwa  hivyo ningependa  kurai kila Mkenya, viongozi, wanasiasa  na  vyombo  vya habari kuwa jeshi letu likijumuisha akina dada na kaka  zetu  hao ndio nguzo  imara na muhimu katika kuendelea na ustawi wetu kama taifa."

 "Hakikisha kuwa lazima tuwe imara na tuweze kuwa makini na kuweza kujiepusha na kuzungumzia   jeshi  kwa  ubaya wowote ule, serikali yangu itajitolea kwa hali na mali kuhakiksha kuwa inalinda jeshi la taifa bila uwoga wala  shauku yoyote '' Rais  Ruto alisema.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved