logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tusker yarejea kileleni mwa jedwali baada ya kuishinda City Stars

Dennis 'Decha' Wanjala alipachika mpira wavuni dakika ya tano.

image
na Tony Mballa

Michezo21 April 2025 - 08:14

Muhtasari


  • Akizungumuza baada ya mechi hiyo, Okere alisema kuwa hawajisikii kuwa na shinikizo licha ya ushindani mkubwa uliopo katika kinyang'anyiro hicho.
  • Akitafakari changamoto za msimu, Okere alionyesha hali ya utulivu na azma.
Wachezaji wa Tusker Dennis Wanjala na Dennis Oguta washerehekea bao lao dhidi ya City Stars ugani Kenyatta, Machakos/Tovuti ya Tusker

Kocha mkuu wa Tusker Charles Okere anaamini wamejipanga kimkakati kutwaa taji msimu huu baada ya kurejea kileleni mwa jedwali la Ligi Kuu ya Kenya Jumapili.

Wanamvinyo hao wa Ruaraka waliimarisha matumaini ya ya kushinda taji lao la 12 kutokana na ushindi wa 1-0 dhidi ya Nairobi City Stars kwenye uga wa Kenyatta mjini Machakos.

Dennis 'Decha' Wanjala alipachika mpira wavuni dakika ya tano na kuipa timu hiyo yenye maskani yake Ruaraka ushindi huo muhimu uliowasukuma hadi alama 51, mbili mbele ya washindani wao wa karibu, Kenya Police.

Akizungumuza baada ya mechi hiyo, Okere alisema kuwa hawajisikii kuwa na shinikizo licha ya ushindani mkubwa uliopo katika kinyang'anyiro hicho.

Akitafakari changamoto za msimu, Okere alionyesha hali ya utulivu na azma. "Imekuwa msimu mgumu kucheza mechi kadhaa bila ushindi lakini tuna furaha hatimaye tumeweza kupata pointi nyingi katika kipindi kigumu sana cha msimu," Okere alisema.

"Ushindani bado ni mkubwa na timu zote tatu za juu zina nafasi sawa kwenye ubingwa lakini tumedhamiria kupambana hadi mwisho," aliongeza.

Okere alisema alibaini kuimarika kwa utendakazi wa kikosi chake baada ya msururu wa matokeo hasi.

“Tulijieleza vyema katika mechi hiyo na ninawaomba wachezaji waendelee na kasi hiyo,” Okere alisema.

Kinyume chake, Nairobi City Stars ilikabiliwa na kipigo cha kutamausha. Kocha msaidizi Peter Opiyo alilalamikia kadi nyekundu iliyotolewa kwa Otieno Omondi dakika ya 54, ambayo aliamini ilivuruga mpango wao wa mchezo.

"Ilitubidi kurejea kwenye ubao wa kuchora na kupanga upya baada ya kadi nyekundu," Opiyo alisema. "Hali ilizidishwa na bao la mapema tulilofungwa kwenye mechi," aliongeza.

Opiyo alisema lengo lao la haraka ni kujinusuru kutoka kwa uwezekano wa kushushwa daraja na kuhifadhi hadhi yao katika daraja la juu msimu ujao.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved