Somalia imemsimamisha kazi afisa michezo kwa sababu ya mwanariadha aliyekimbia kwa kasi ya chini

Uchunguzi wa wizara ya jijana na michezo ya Somalia ulifichua kuwa "si mtu mwanamichezo, wala si mkimbiaji".

Muhtasari
  • Mwenyekiti wa Shirikisho la Riadha la Somalia ameshutumiwa kwa kutumia vibaya mamlaka yake na kuiaibisha Somalia.
  • Khadijo Aden Dahir alisimamishwa kazi kufuatia mkutano kati ya wizara ya michezo ya nchi hiyo na kamati yake ya kitaifa ya Olimpiki.
Image: BBC

Somalia imemsimamisha kazi afisa wa michezo kwa upendeleo baada ya mwanariadha novice kuruhusiwa kushiriki mashindano ya kimataifa ya michezo.

Nasra Abubakar Ali alichukua karibu mara mbili ya muda wa mshindi kumaliza mbio za mita 100 katika mashindano ya michezo ya Vyuo Vikuu vya Dunia yaliyofanyika nchini China.

Uchunguzi wa wizara ya jijana na michezo ya Somalia ulifichua kuwa "si mtu mwanamichezo, wala si mkimbiaji".

Mwenyekiti wa Shirikisho la Riadha la Somalia ameshutumiwa kwa kutumia vibaya mamlaka yake na kuiaibisha Somalia.

Khadijo Aden Dahir alisimamishwa kazi kufuatia mkutano kati ya wizara ya michezo ya nchi hiyo na kamati yake ya kitaifa ya Olimpiki.

Uchunguzi wao wa awali pia uligundua kuwa shirika la michezo linalojulikana kama Chama cha Michezo cha Chuo Kikuu cha Somalia halipo.

Wizara hiyo ilisema itafuatilia hatua za kisheria dhidi ya mwenyekiti wa Shirikisho la Riadha la Somalia na wengine waliohusika na "udanganyifu" katika kikundi cha michezo.

Haikufafanua zaidi uhusiano kati ya Bi Dahir na Bi Ali ni upi.

Katika video ya tukio hilo, mwanariadha huyo akiachwa mbali na wanariadha wengine na mwishowe anakamilisha mbio kwa kuruka kwa furaha.

Mwanariadha huyo alimaliza mbio kwa sekunde 21.81 - zaidi ya sekunde 10 nyuma ya mshindi wa mwisho.

Waziri wa Michezo Mohamed Barre Mohamud alitaja tukio hilo kuwa la aibu.

"Kilichotokea leo si uwakilishi wa watu wa Somalia... tunaomba radhi kwa watu wa Somalia," alisema.

Ukweli kwamba aliripotiwa kuwa hakuwa na uzoefu wa awali wa kushindana umewafanya baadhi ya Wasomali kushangaa kwa nini alichaguliwa kushiriki mashindano hayo.

Article share tools