logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sijashuhudia kisa chochote cha kuwahonga wapiga kura-Malala

Aidha alitoa wito kwa wapiga kura kujitokeza kwa wingi kwenye uchaguzi huo.

image

Uchaguzi29 August 2022 - 12:17

Muhtasari


  • Malala amesema kuwa hajashuhudia kisa chochote cha kuwahonga wapiga kura, akidokeza kuwa uchaguzi huu ni wa amani
Seneta wa Kakamega Cleophas Malala

Muwaniaji wadhifa wa Ugavana wa Kakamega Cleophas Malala  amejitenga na madai ya kuwahonga wapiga kura katika uchaguzi wa Ugavana unaoendelea.

Malala amesema kuwa hajashuhudia kisa chochote cha kuwahonga wapiga kura, akidokeza kuwa uchaguzi huu ni wa amani.

Alitoa wito kwa viongozi kukoma kuwachochea wakazi kwa kutoa matamshi ambayo hayana msingi, akiwataka walio na malalamishi kuripoti kwa afisi husika.

Malala, aliwapongeza wakazi kwa kudumisha amani katika uchaguzi unaoendelea wa gavana kakamega.

“Tumeshuhudia hali ya amani, nawashukuru watu wa Kakamega kwa kushiriki ucaguzi wa amani. Ni muhimu kwa wakazi kuruhusiwa kupiga kura kuwachagua viongozi wao,” alisema Malala.

Aidha alitoa wito kwa wapiga kura kujitokeza kwa wingi kwenye uchaguzi huo.

Malala alisema atakubali kushindwa iwapo uchaguzi hautakumbwa na changamoto huku akitoa wito kwa wapinzani wake kukubali matokeo.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved