logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Wapenzi Waliotazamia Kufunga Ndoa Watenganishwa Baada Ya Wazazi Wa Mwanadada Kukataa Mahari

Ednah alifichua kwamba wakati alipopatana na Wambua, alikuwa na ujauzito wa mpenziwe wa awali ambaye alifariki.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho06 February 2025 - 08:39

Muhtasari


  • Ednah alisema uhusiano wao wa mwaka mmoja ulivunjika Julai 2022 baada ya wazazi wake kukataa kuchukua mahari ya Wambua.
  • “Nilishamove on kitambo. Nilishamueleza. Alinipigia juzi akanisalimia tu,” Wambua alisema.

Warangazaji

Mwanadada aliyejitambulisha kama Ednah Mutheu (23) kutoka Machakos alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na aliyekuwa mpenzi wake, Albanus Wambua (30) ambye alikosana naye takriban miaka mitatu iliyopita.

Ednah alisema uhusiano wao wa mwaka mmoja ulivunjika Julai 2022 baada ya wazazi wake kukataa kuchukua mahari ambayo Wambua alitaka kupeleka nyumbani kwao ili amuoe.

Aidha, alifichua kwamba wakati alipopatana na Wambua, alikuwa na ujauzito wa mpenziwe wa awali ambaye alifariki.

“Tulipatana naye Facebook. Nikapata kumbe sio wa mbali sana na kwetu. Wakati huo nilikuwa katika chuo cha KMTC. Baby daddy wangu alipata ajali akafariki dunia,” Ednah alisimulia.

“Baada ya kupatana Facebook, akasema anataka bibi. Wakati huo sikumwambia niko na mimba. Nilikuja kumwambia baadaye baada ya kujuana. Hakukataa, alisema watoto tutapata. Wakati ukafika akasema anataka kupeleka mahari lakini wazazi wakakataa wakasema kwanza nimalize shule,” aliongeza.

Ednah alisema kwamba baada ya kumaliza shule hajaweza kuelewana na mpenziwe huyo kuhusu suala la ndoa.

“Sasa nimemaliza shule tayari. Nimekuwa nikimtafuta lakini anablock simu zangu. Kama ashamove ni sawa nitakubali, kama hajamove on nitamuomba msamaha juu nilimkosea. Mimi nilimuona ni jamaa mzuri ambaye ananipenda. Ata akinikataa ni sawa. Mtoto ako na miaka tatu, namshughulikia nyumbani,” alisema.

Wambua alpipogiwa simu, hakusita kueleza kwamba tayari amesonga mbele na maisha yake.

“Nilishamove on kitambo. Nilishamueleza. Alinipigia juzi akanisalimia tu,” Wambua alisema.

Ednah alisema, “Hakuniambia ashamove on. Aliniambia niende nimalize shule nitapata akiwa single.”

Hata hivyo, hakuwa na budi ila kukubali msimamo wa Wambua.

“Niko sawa, lakini sio sawa. Nilikuwa na matumaini lakini kama imekuwa hivyo ni sawa,” alisema.

 Alimwambia Wambua, “Asante kwa yote ulinifanyia. Nakuombea uishi vizuri na familia yako. Uniombee nipate mtu mzuri kama wewe niweze kuishi na Amani.”

Wambua alimwambia, “Namtakia mema kwa maisha yake.”


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved