logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: "Nataka amani!" Kijana alia kutengwa na babake mzazi baada ya kukosana na mamake

"Mzee alifika mahali akasema mimi sio mtoto wake. Alisema hatutaki juu amekosana na mama," Benson alisema.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho06 March 2025 - 08:39

Muhtasari


  • Benson alisema mzazi wake alimkana yeye na ndugu zake baada ya uhusiano wake na mama yao kukosana miaka mingi iliyopita.
  • Kijana huyo alisema angependa kurejesha uhusiano na mzazi wake ili kupata amani moyoni.

Warangazaji

Benson Andole, mwenye umri wa miaka 24, kutoka Kakamega alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na baba mzazi wake Festus Muchesia (65) ambaye alimtengana baada ya kukosana na mamake.

Benson alisema mzazi wake alimkana yeye na ndugu zake baada ya uhusiano wake na mama yao kukosana miaka mingi iliyopita.

Hii ilimlazimu kulelewa na nyanya yake hadi alipofariki akiwa kijana mdogo.

“Baba alikosana na mama yangu. Mzee alifika mahali akasema mimi sio mtoto wake. Alisema hatutaki juu amekosana na mama. Tulilelewa na nyanya yangu. Nyanya alipokufa alisema nirudi kwa boma. Baada ya kukaa na yeye mwaka moja akatufukuza. Nikasema niondoke nikarudi kwa momba wangu nikakaa huko. Ilifika mahali nikapata kazi,” Benson alisema.

Kijana huyo alisema angependa kurejesha uhusiano na mzazi wake ili kupata amani moyoni.

“Imefika mahali nikasema nataka amani. Kama ni shamba sitaki, nataka amani. Nataka tuwe kitu kimoja, kama ni vitu vingine nitatafuta mwenyewe. Ametenga dada yangu na pia kaka yangu wa huyo mama mwingine. Ametutenga wote,” alisema.

Bwana Festus alipopigiwa simu alimtaja mwanawe huyo kama mtoto mtukutu, ambaye ni tofauti sana na ndugu zake.

“Kichwa yake ilikuwa tofauti. Nilitaka hata asome Polytechnic ikashindikana. Alikuja akanitusi, sikutaka hiyo maneno. Alinitukana mpaka anaandika meseji mbaya nikasema mimi sitaki,” Bw Festus alisema kabla ya kukata simu.

Benson alikanusha madai ya mzazi wake kwamba yeye ni mtukutu, na akasisitiza jinsi mzee huyo alivyomtenga.

“Alitufukuza nikiwa na mwaka mmoja. Kutoka wakati huo ni nyanya yangu alifunza hadi alipofariki. Mimi sikumtusi. Meseji nilimwandikia nilimwambia dadangu anasumbuka huku na asitutenge hadi kama alikosana na mama. Nikimpigia hawezi chukua simu. Mwaka jana aliita mama na mjomba akasema anataka kurejesha watoto wake hata kama alikosana naye,” alisema.

Bwana Festus alipigiwa simu tena lakini akaweka wazi kwamba hako tayari kurejesha uhusiano na mwanawe.

Benson alimalizia kwa kusema, “Baba mimi nakufahamu kama mzazi. Nilkuwa nataka Amani turejeshe mawasiliano, na pia niweze kupata baraka zako na niweze kusaidia ndugu zangu wakati nikiimarika.”

Je, una ushauri ama maoni gani kuhusu Patanisho ya leo?


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved