Leo hii katika kitengo cha patanisho bwana Frank alituma ujumbe ii apatanishwe na mkewe mama Jayden ambaye wamekuwa kwa ndoa kwa miaka miwili.
"Tulikosana na mke wangu mwezi jana baada ya yangu kutoka nje ya ndoa, baada ya mke wangu kujifungua kulikuwa na shida nilimpa miezi sita ili aweze kupona
baada ya kupona mke wangu hakuwa na hamu ya tendo ya ndoa, jambo hilo ndilo lilinikusudia na kunichangia niende nje ya ndoa lakini nilikuwa nafanya kimaksudi ili mke wangu aweze kuona kuwa ananitesa
Pia alibadilika kabisa hata hakuwa ananipikia kiamsha kinywa, na mshawishi lakini hakuweza kunisikia
Naomba turudiane kwa maana ninaumia sana na mambo hutendeka." Alieleza Frank.