logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Je, sarakasi za Embarambamba zinahatarisha maisha yake?

Embarambamba amewachilia video mpya inayomshirikisha kukimbia kwenye barabara iliyo na magari

image
na Radio Jambo

Habari20 May 2021 - 06:03

Muhtasari


Embarambamba amewachilia video mpya inayomshirikisha kukimbia kwenye barabara iliyo na magari

Embarambamba akiwa kwenye sarakasi zake

Wimbo mpya wa msanii wa nyimbo za injili, Christopher Nyangwara, almaarufu kama Embarambamba ‘nimeanza safari’ umepokelewa na hisia mbalimbali.

Video ya mwanamuziki huyo akinusurika kugongwa na bodaboda iliyokuwa ikisambazwa mtandaon kabla ya kutolewa kwa wimbo iliibua gumzo sana mtandaoni huku Wakenya wakimwagiza Embarambamba kuwa makini anapocheza sarakasi zake.

Kwenye wimbo huo uliowekwa kwenye mtandao wa Youtube siku ya jumanne, mwanamuziki huyo mwenye mitindo ya densi ya  kustaajabisha  ameonekana kukimbia kwenye barabara iliyo na magari kutoka upande mmoja hado mwingine huku magari yakipita.

Mwanamuziki huyo tokea Nyamira amepata umaarufu mkubwa mno kutokana na sarakasi zinazoambatana na densi zake. Wengi wamestaajabishwa na sarakasi zile huku wengine wakikisia kwamba huenda anahitaji huduma za mtaalamu wa kisaikolojia.

Embarambamba ameendelea kupata umaarufu mkubwa huku akipata mikataba na baadhi ya kampuni tajika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved