logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pasta Ng’ang’a Akutana na CS Alice Wahome Kujadili Kuhusu ‘Affordable Housing’

Mkutano wao umetokea wiki chache baada ya Ng’ang’a kusutwa kwa kumfukuza Milka Moraa Tegisi kanisani na kumtaka kuenda kwa serikali kutafuta msaada

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani12 February 2025 - 14:41

Muhtasari


  • Waziri alisema lengo la serikali ni kujenga nyumba takribani milioni moja katika kipindi cha miaka 5 ijayo.
  • “Lengo letu ni kubwa lakini linaweza kufikiwa: kutoa nyumba milioni 1 katika miaka mitano ijayo, na kufikia zaidi ya Wakenya milioni 15." 

CS Alice Wahome akutana na Pasta Ng'ang'a

WAZIRI wa Ardhi, Alice Wahome amekutana na mchungaji James Maina Ng’ang’a wa kanisa la Neno Evangelism, siku kadhaa baada ya pasta huyo kumfukuza mwanamke kanisani na kumtaka kutafuta usaidizi wa serikali.


Katika chapisho lake kupitia ukurasa wa Facebook, CS Wahome alifichua kwamba Ng’ang’a alimtembelea katika ofisi yake kujadili masuala ibuka kuhusu mradi wa serikali wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu.


“Asubuhi ya leo, Mtume James Maina Ng’ang’a amenitembelea kwa ukarimu ili kujadili Mpango wa Serikali wa Nyumba Nafuu. Ushirikiano huu ni sehemu ya juhudi zetu zinazoendelea za kuelimisha na kujenga ufahamu miongoni mwa Wakenya kuhusu fursa zinazopatikana kupitia mpango huu wa kuleta mabadiliko,” Wahome alisema.


Waziri huyo alisema kwamba mchungaji Ng’ang’a alikuwa na uchu wa kutaka kujua jinsi mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu unaonyesha kuongezeka kwa uelewa na msaada kutoka sekta mbalimbali za jamii.


“Ziara ya Mtume Ng’ang’a ni ya kutia moyo na yenye athari. Nia yake ya kuelewa programu inaonyesha kuongezeka kwa ufahamu na usaidizi kutoka kwa sekta mbalimbali za jamii. Wakati wa majadiliano yetu, nilijitolea kumwongoza katika mchakato wa kupata nyumba za bei nafuu na kumfundisha kuhusu muundo na manufaa ya program,” CS Wahome alisema.


Waziri alisema lengo la serikali ni kujenga nyumba takribani milioni moja katika kipindi cha miaka 5 ijayo.


“Lengo letu ni kubwa lakini linaweza kufikiwa: kutoa nyumba milioni 1 katika miaka mitano ijayo, na kufikia zaidi ya Wakenya milioni 15 moja kwa moja na kwa njia zisizo za moja kwa moja,” alisema.


Mkutano wao umetokea wiki chache baada ya Ng’ang’a kusutwa kwa kumfukuza Milka Moraa Tegisi kanisani na kumtaka kuenda kwa serikali kutafuta msaada baada ya kuomba msaada wa kodi ya nyumba.


 


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved