logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Muonekano Mpya Wa Salasya Baada Ya Kudai Kufanya Upasuaji Wa Midomo (Video)

Kwa mujibu wa Cleveland Clinic, Upasuaji wa midomo maarufu kama ‘Lip Augmentation’ huongeza unene kwa midomo nyembamba, na kuunda kuonekana zaidi kwa ujana.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani18 February 2025 - 08:51

Muhtasari


  • “Ndio naendelea kupata nafuu baada ya upasuaji mdogo wa midomo. Sasa hivi midomo yangu inakaa kama ya yule Mrembo wa Tanzania, Madonna,” alisema.

MP Peter Salasya aonyesha muonekano mpya baada ya kudai kufanyiwa upasuaji wa midomo

MBUNGE wa Mumias Mashariki Peter Salasya amewakosha watumizi wa mitandao ya kijamii baada ya kuonyesha muonekano wake mpya kwenye video fupi aliyopichapisha.

Katika video hiyo, Mbunge huyo anayejitambulisha kama ‘Gen Z’ alionesha video hiyo akiwa amevimba midomo na kufichua kwamba alifanyiwa upasuaji.

Salasya alitania kwamba ndio ameanza safari ya kupata nafuu baada ya upasuaji mdogo kwenye midomo yake na kutania kwamba midomo yake sasa imekuwa mikubwa kama ya mwanashosholaiti Fulani kutoka Tanzania.

“Ndio naendelea kupata nafuu baada ya upasuaji mdogo wa midomo. Sasa hivi midomo yangu inakaa kama ya yule Mrembo wa Tanzania, Madonna,” alisema.

Hata hivyo, baadhi walihisi kwamba alikuwa anamrejelea Mrembo wa huku Kenya Tanasha Donna ambaye mwaka jana alionyesha muonekano wake mpya baada ya kuboresha muonekano wa midomo yake.

Wengine walihisi kwamba mbunge huyo alikuwa anazua utani tu kwa kutumia teknolojia za kisasa kama vile akili mnemba (AI) kuhariri muonekano wake, wakihisi kwamba sio kweli kuhusu kufanya sajari ya midomo.

Kwa mujibu wa Cleveland Clinic, Upasuaji wa midomo maarufu kama ‘Lip Augmentation’ huongeza unene kwa midomo nyembamba, na kuunda kuonekana zaidi kwa ujana.

Kuna aina kadhaa za kuongeza midomo, ikiwa ni pamoja na kujaza midomo, vipandikizi, uhamisho wa mafuta na kuinua midomo. Wakati wa kurejesha, matokeo na hatari zinazowezekana hutofautiana kwa kila utaratibu.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved