
MREMBO mmoja amechukua kwenye TikTok kuelezea jambo la ajabu wakati waligundua kwamba ajuza wao mwenye umri wa miaka 76 ana mimba.
Hadithi ilishirikiwa kwenye jukwaa la
kushiriki video, TikTok na mwana mtandao aliyetambulika kama Ammielewis.
Kulingana naye, mamake alikuwa akijisikia
vibaya kidogo, na alipopelekwa hospitalini, iligundulika kwamba alikuwa na
ujauzito wa wiki 12.
Habari hizo ziliiacha familia yao katika
mshangao na mama yake, alifichua, ameamua kumweka mtoto huyo.
Aliandika…
“Nilipogundua kuwa mama yangu mwenye
umri wa miaka 76 aligundulika kuwa na ujauzito wa wiki 12, nilishtuka.”
“Mama yangu amekuwa na nguvu kila
wakati lakini hakuna mtu aliyetarajia angekuwa mjamzito katika umri kama huo.
Yote ilianza alipoenda hospitali kutokana na kizunguzungu. Familia nzima
ilikuwa katika kutoamini. Hatukuweza kuelewa jinsi angeshughulikia hili katika
uzee kama huo na ni nani angemlea mtoto.”
“Mama yangu alichukua uamuzi wa kulea
mimba licha ya umri wake na mashaka yetu yote. Aliamua kuwa mama mkubwa zaidi
katika historia.”
“Nilianza kutambua kwamba yeye
haogopi kuwa mfano kwetu. Kwa maana mama yangu amekuwa akipigania maisha yake
na sasa yuko tayari kupigania mustakabali wa mtoto huyu."
Lakini je, mwanamke anaweza beba ujauzito
akiwa na umri wa zaidi ya miaka 50?
Kwa mujibu wa MedicineNet, Ndiyo, mwanamke
anaweza kupata mimba akiwa zaidi ya umri wa miaka 70 kwa msaada wa matibabu,
lakini hatari huongezeka kwa umri.
Hata hiyo, madaktari wanashauri kwamba mimba
hizi kwa kawaida hutimizwa kwa mayai ya wafadhili na urutubishaji katika mfumo
wa uzazi (IVF).
Hakuna umri wa uzee uliowekwa ambapo
unaweza kupata mjamzito kwa kawaida, lakini uzazi huanza kupungua kadiri
unavyozeeka.