logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maajabu Ajuza Mwenye Umri Wa Miaka 76 Akipata Ujauzito

Kulingana naye, mamake alikuwa akijisikia vibaya kidogo, na alipopelekwa hospitalini, iligundulika kwamba alikuwa na ujauzito wa wiki 12.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani23 February 2025 - 10:19

Muhtasari


  • Hadithi ilishirikiwa kwenye jukwaa la kushiriki video, TikTok na mwana mtandao aliyetambulika kama Ammielewis.
  • Kulingana naye, mamake alikuwa akijisikia vibaya kidogo, na alipopelekwa hospitalini, iligundulika kwamba alikuwa na ujauzito wa wiki 12.
  • Habari hizo ziliiacha familia yao katika mshangao na mama yake, alifichua, ameamua kumweka mtoto huyo.

Mimba

MREMBO mmoja amechukua kwenye TikTok kuelezea jambo la ajabu wakati waligundua kwamba ajuza wao mwenye umri wa miaka 76 ana mimba.

Hadithi ilishirikiwa kwenye jukwaa la kushiriki video, TikTok na mwana mtandao aliyetambulika kama Ammielewis.

Kulingana naye, mamake alikuwa akijisikia vibaya kidogo, na alipopelekwa hospitalini, iligundulika kwamba alikuwa na ujauzito wa wiki 12.

Habari hizo ziliiacha familia yao katika mshangao na mama yake, alifichua, ameamua kumweka mtoto huyo.

Aliandika…

“Nilipogundua kuwa mama yangu mwenye umri wa miaka 76 aligundulika kuwa na ujauzito wa wiki 12, nilishtuka.”

“Mama yangu amekuwa na nguvu kila wakati lakini hakuna mtu aliyetarajia angekuwa mjamzito katika umri kama huo. Yote ilianza alipoenda hospitali kutokana na kizunguzungu. Familia nzima ilikuwa katika kutoamini. Hatukuweza kuelewa jinsi angeshughulikia hili katika uzee kama huo na ni nani angemlea mtoto.”

“Mama yangu alichukua uamuzi wa kulea mimba licha ya umri wake na mashaka yetu yote. Aliamua kuwa mama mkubwa zaidi katika historia.”

“Nilianza kutambua kwamba yeye haogopi kuwa mfano kwetu. Kwa maana mama yangu amekuwa akipigania maisha yake na sasa yuko tayari kupigania mustakabali wa mtoto huyu."

Lakini je, mwanamke anaweza beba ujauzito akiwa na umri wa zaidi ya miaka 50?

Kwa mujibu wa MedicineNet, Ndiyo, mwanamke anaweza kupata mimba akiwa zaidi ya umri wa miaka 70 kwa msaada wa matibabu, lakini hatari huongezeka kwa umri.

Hata hiyo, madaktari wanashauri kwamba mimba hizi kwa kawaida hutimizwa kwa mayai ya wafadhili na urutubishaji katika mfumo wa uzazi (IVF).

Hakuna umri wa uzee uliowekwa ambapo unaweza kupata mjamzito kwa kawaida, lakini uzazi huanza kupungua kadiri unavyozeeka.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved