logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Salasya Ataja Sababu Zitakazompeleka Mbinguni Baada Ya Kutumikia Kenya Kama Rais

“Nitaenda mbinguni baada ya kutumikia nchi yangu ya Kenya kwa bidii. Nitakuwa rais bora wa kenya nimepata tangu uhuru, Nitamshida hata Kibaki” Salasya alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani24 February 2025 - 10:02

Muhtasari


  • Mbunge huyo ambaye yuko bungeni kwa muhula wake wa kwanza amekuwa akidokeza kuhusu nia yake ya kuliwakilisha taifa la Kenya katika wadhifa wa juu zaidi 

MP Peter Salasya

MBUNGE wa Mumias Mashariki, Peter Salasya amesema anafikiri ucheshi, upekee, akili, na hekima nyingi aliyo nayo zitakuwa sababu kuu za kumfanya kuenda mbinguni baada ya kutumikia taifa kama rais siku za usoni.

Mbunge huyo wa chama cha DAP-K alisema haya wikendi iliyopita wakati akizungumza na wapiga kura wake katika eneo bunge lake kaunti ya Kakamega.

Salasya alisema kwamba vigezo hivyo vitamfanya kuwa miongoni mwa wachache ambao watakwenda mbinguni huku akijipigia debe kuwa rais mzuri zaidi ambaye atalihudumia taifa tangu Kenya kuzaliwa mwaka 1963.

“Nadhani mimi ni mcheshi wa kipekee mwenye akili na hekima ya Mungu. Nitaenda mbinguni baada ya kutumikia nchi yangu ya Kenya kwa bidii. Nitakuwa rais bora wa kenya nimepata tangu uhuru,” Salasya alisema.

Mbunge huyo bila kutaja atakuwa rais wa awamu ya ngapi, alisisitiza kwamba atakuwa rais mchapakazi kumshinda marehemu Mwai Kibaki – rais wa 3 anayetajwa kuwa rais aliyeleta mabadiliko makubwa ya kimaendeleo nchini kati ya 2007 na 2013.

“Nitamshida hata Kibaki kwa sababu ya moyo wangu mzuri wa kumtumikia kila mtu na kuona nchi yangu taifa langu likiwa na nguvu na bora nitakuwa rais wa kihistoria ambaye sitasahaulika kwa miaka 1,000 ijayo,” aliongeza.

Mbunge huyo ambaye yuko bungeni kwa muhula wake wa kwanza amekuwa akidokeza kuhusu nia yake ya kuliwakilisha taifa la Kenya katika wadhifa wa juu zaidi nchini katika siku za mbeleni.

Salasya amekuwa ni mwiba katika uongozi wa serikali ya Ruto, ambapo kutoka ukanda wa Magharibi mwa Kenya ni miongoni mwa wachache wanaosimama na kupinga sera za Kenya Kwanza wazi wazi.

Mwezi jana wakati wa ziara ya siku 5 ya kimaendeleo ya rais Ruto katika ukanda huo, Salasya alimwambia bayana kuhusu changamoto za bima ya mataifa, SHA akisema kwamba rais haambiwi ukweli.

Salasya alimtaka Ruto kumpa nafasi ya kuwa mshauri wake kuhusu mambo ya kweli kwenye ‘ground’ haswa kuhusu SHA.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved