logo

NOW ON AIR

Listen in Live

‘Red Flag’: Mrembo Aonya Wanawake Dhidi Ya Ku’date Wanaume Wanaojua Kupika

Kwa mjibu wa mwanadada huyo, mwanamume yeyote ambaye ni fundi katika masuala ya jikoni ni ‘red flag’ kubwa sana, akisema kuwa hao mara nyingi ndio huwa sumu kuishi nao.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani25 February 2025 - 14:15

Muhtasari


  • Kwa mjibu wa mwanadada huyo, mwanamume yeyote ambaye ni fundi katika masuala ya jikoni ni ‘red flag’ kubwa sana, akisema kuwa hao mara nyingi ndio huwa sumu kuishi nao.
  • Mwenyewe, alisema kuwa hawezi kubali posa kwa mwanamume anayejua kupika hata kwa mtutu wa bunduki.

Mrembo akataza dhidi ya kuolewa na mwanamume anayejua kupika

MWANAMKE mmoja mwenye umri wa makamo amezua gumzo katika mitandao wa X baada ya kuibua tetesi kwamba wanaume wanaojua kupika kuwa nao katika mahusiano ni kujikosea heshima kama mwanamke.

Katika video hiyo ambayo imegawanya wachangiani maoni kwa makundi mawili, Mrembo huyo alianza akisema kwamba anawaonea huruma sana wanawake walioko kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanaume ambao ni wapishi wazuri.

Kwa mjibu wa mwanadada huyo, mwanamume yeyote ambaye ni fundi katika masuala ya jikoni ni ‘red flag’ kubwa sana, akisema kuwa hao mara nyingi ndio huwa sumu kuishi nao.

“Unapoolewa na mwanamume anayeweza kupika ni red flag. Wakati nyinyi mnapigana, atapika, atakula, atafurahi na kwenda kulala.”

“Hakuna kisingizio cha yeye kukubembeleza. Hasa ikiwa anaweza kupika zaidi yako na pia kujua jinsi ya kuweka ubaya, utateseka katika uhusiano huo,” alisema.

Aliongeza akitoa onyo kwa wanawake kutofanya uthubutu wa kuolewa na mwanamume anayejua kupika, akiita hatua hiyo kama moja kati ya makosa makubwa ambayo mwanamke yeyote anayejipenda atafanya.

Mwenyewe, alisema kuwa hawezi kubali posa kwa mwanamume anayejua kupika hata kwa mtutu wa bunduki.

“Usijaribu kuingia katika uhusiano na mwanamume anayejua kupika, hata mimi mwenyewe siwezi kubali mwanamume wangu awe hodari jikoni. Kupika ni biashara yangu tu,” aliongeza.

Tazama video hiyo hapa chini jinsi watu waliweza kuchangia maoni kwenye jambo hilo;

×

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved