logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kumbatia Kalamu Na Busu Vitabu Badala Ya Mapenzi – Babu Owino Ashauri Wanafunzi

“Kama utambusu mwanamume, basi busu kitabu. Na kama utamkumbatia mwanamke basi kumbatia kalamu,” Owino aliongeza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani05 March 2025 - 12:34

Muhtasari


  • Owino alitumia lugha fiche kuwataka kuzingatia zaidi kalamu na vitabu vyao badala ya kukumbatia na kubusu wenzao wa jinsia tofauti shuleni.

Babu Owino

MBUNGE wa Embakasi Mashariki, Babu Owino ametoa ushauri kwa wanafunzi huku wanaporejea shuleni baada ya likizo fupi ya katikati mwa muhula wa kwanza.

Akizungumza bungeni wakati wanafunzi wa shule moja kutoka Embakasi walipozuru majengo ya bunge, Owino ambaye alipewa nafasi ya kutoa ushauri kwa wanafunzi hao na naibu spika Gladys Shollei aliwataka kutoendekeza mapenzi masomoni.

Owino alitumia lugha fiche kuwataka kuzingatia zaidi kalamu na vitabu vyao badala ya kukumbatia na kubusu wenzao wa jinsia tofauti shuleni.

“Kwa niaba ya mheshimiwa Mawathe, ningependa kuchukua nafasi hii kuwakaribisha wanafunzi kutoka Eneobunge la Embakasi Kusini na ninataka kuwapa neno la ushauri kama watoto wetu,” Owino alisema.

“Elimu ndio njia pekee kuelekea mafanikio. Mizizi ya masomo ni michungu lakini matunda yake ni matamu. Wavulana kwa wasichana kumbuka ukiwa shuleni sasa hivi zingatia kwenye vitabu na kalamu.”

“Kama utambusu mwanamume, basi busu kitabu. Na kama utamkumbatia mwanamke basi kumbatia kalamu. Hicho ndicho kitu pekee ambacho kitakuokoa kutoka katika lindi la umaskini,” Owino aliongeza.

Video hiyo hiyo ambayo imevutia maoni mengi ya vichekesho ndio hii hapa chini;

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved