logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanawe Museveni, Muhoozi Kainerugaba, afichua jinsi wanawake wamemfanya aepuke kanisa

Muhoozi anasema uwepo wa wanawake warembo kanisani ni shida kwani ni majaribio makubwa kwake.

image
na Samuel Mainajournalist

Burudani11 March 2025 - 09:46

Muhtasari


  • Kupitia jumbe zake za Jumanne asubuhi, Muhoozi alieleza kuwa yeye huomba akiwa kambini na wanajeshi wake badala ya kanisani.
  •  Muhoozi alisema hawezi kuwa padre kwa sababu hana uwezo wa kuachana na wanawake na kumlenga Mungu pekee.

Muhoozi Kainerugaba

Jenerali Muhoozi Kainerugaba, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda (UPDF) na mwana wa Rais Yoweri Museveni, amefichua sababu tata inayomfanya kuepuka kuhudhuria ibada za kanisa.

Kupitia jumbe zake za Jumanne asubuhi, Muhoozi alieleza kuwa yeye huomba akiwa kambini na wanajeshi wake badala ya kanisani.

Sababu kuu ya hili, anasema, ni uwepo wa wanawake warembo kanisani ambao anaamini ni majaribio makubwa kwake.

"Ndiyo maana ninaepuka ibada za kanisani kwa makusudi. Kuna wanawake wengi warembo sana huko. Ni kama shetani anawaleta wote kwa ajili yangu. Hapana, mimi huomba kambini na wanajeshi wangu. Huko tunaweza kumlenga Mungu kikamilifu!" aliandika Muhoozi kwenye akaunti yake ya Twitter.

Kauli yake ilikuja baada ya mwanawe Museveni kudai kwamba kuwa mwanajeshi ni moja ya uamuzi bora kwa mwanaume, lakini akasisitiza kuwa hatua bora zaidi ni kuwa padre—kumtumikia Mungu kikamilifu.

Hata hivyo, alisema kwamba yeye hawezi kuwa padre kwa sababu hana uwezo wa kuachana na wanawake na kumlenga Mungu pekee.

"Zamani nilisoma mahali kwamba kuwa mwanajeshi ni jambo la pili bora zaidi kwa mwanaume. Jambo bora kabisa ni kuwa padre, kumtumikia Mungu kwa moyo wote, kuachana na wanawake na kumlenga Mungu pekee. Niliposikia suala la kuachana na wanawake, nilijua siwezi," alisema.

Muhoozi, ambaye anajulikana kwa kauli zake tata kwenye mitandao ya kijamii, alijivunia kuwa na wafuasi wengi wa kike, akiwataja kama viumbe warembo zaidi walioumbwa na Mungu.

Pamoja na hayo, alihimiza vijana wa Uganda na Afrika kwa ujumla kujiunga na jeshi ili kufurahia faida za maisha ya kijeshi.

"Kwa vijana wa Uganda na Afrika, huwezi kuwa mwanaume kamili kama hujawahi kuhudumu jeshini. Hilo haliwezekani," alisisitiza.

Muhoozi alifafanua kuwa ili mtu ajiunge na jeshi la Uganda, anahitaji kuwa na afya njema, kuwa raia wa Uganda, kuwa na nidhamu na elimu inayohitajika.

"Kama kuna afisa wa UPDF anayekutaka utoe pesa ili akuajiri, niambie jina lake hapa na ataona cha mtema kuni," alionya.

Muhoozi ameendelea kuvutia mijadala kutokana na matamshi yake yenye utata kwenye mitandao ya kijamii, huku wengine wakimtazama kama mrithi wa baba yake katika siasa za Uganda.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved