logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Goliath wa Bungoma: Nilifungwa jela kwa mwezi 1 baada ya kupoteza pikipiki ya mkopo

“Karo ilileta shida nikaachia tu darasa la nne. Kutoka hapo nikaanza kuchimba miti ya kuchoma makaa, nikaanza kujituma katika vibarua vingine kama kuchungia watu ng’ombe,” Otesa alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani24 April 2025 - 08:59

Muhtasari


  • Baba huyo wa watoto 3 mwenye umri wa miaka 29 alieleza kwamba maisha yake ya utotoni hayakuwa rahisi kwani alilazimika kuachia shule katika darasa la 4 kutokana na kukosekana kwa karo.
  • Baada ya kuacha shule, Otesa alianza vibarua vya kuchoma makaa na baadae akajitosa katika biashara ya usafiri wa umma kwa kutumia bodaboda.

Isaac Otesa maarufu kama Goliath wa Bungoma//Screengrab-TV47 YouTube

ISAAC Otesa maarufu kama Goliath wa Bungoma kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu maisha yake ya kabla ya umaarufu.


Akizungumza kwenye runinga ya TV47 na Dr Ofweneke, Otesa Alifichua kwamba kabla ya umaarufu wa ghafla shukrani kwa Maandamano ya vijana wa Gen Z, alikuwa anahangaika na maisha ya kijijini.


Baba huyo wa watoto 3 mwenye umri wa miaka 29 alieleza kwamba maisha yake ya utotoni hayakuwa rahisi kwani alilazimika kuachia shule katika darasa la 4 kutokana na kukosekana kwa karo.


Baada ya kuacha shule, Otesa alianza vibarua vya kuchoma makaa na baadae akajitosa katika biashara ya usafiri wa umma kwa kutumia bodaboda.


“Karo ilileta shida nikaachia tu darasa la nne. Kutoka hapo nikaanza kuchimba miti ya kuchoma makaa, nikaanza kujituma katika vibarua vingine kama kuchungia watu ng’ombe,” Otesa alisema.


Hata hivyo, katika biashara ya bodaboda, alipatwa na majanga wakati pikipiki aliyekuwa ameichukua kwa mkopo ilipopotea katika mazingira tatanishi kumpelekea yeye kufungwa jela.


“Baadae niliingia kwa pikipiki ya mtu nikaanza kumuendeshea pole pole kisha nikaingia kwa chama nikachukua mkopo. Baadae ile pikipiki ilikuja ikapotea nikashikwa nikafungwa jela kwa kipindi cha mwezi mmoja,” Otesa Alifichua.


Baada ya kesi kukamilika, alirudi uraiani na kuanza maisha upya kwa kuendesha pikipiki ya mtu mwingine tena.


“Mungu alinisaidia ile kesi ikakamilika sikufungwa tena, nikitoka Mungu akafungua njia nikapata pikipiki ya mtu tena na hivyo hivyo hadi pale hizi harakati za Gen Z zilipoanza na nikajipata kwenye mwanga wa umma,” Isaac Otesa alisema.


Alisema kwamba hakujua kwamba kuna jamaa mwingine – Bradley Marongo – ambaye walikuwa na mfanano kama riale kwa ya pili.


Kulingana naye, wakati Bradley alionekana Nairobi kwenye Maandamano, yeye alikuwa Bungoma akijishughulisha na biashara ya pikipiki wakati polisi wa Trafiki mmoja alimdokezea kwamba ameona mtu kama yeye Nairobi.


“Mimi niko Bungoma, ikasemekana kwamba niko Maandamano Nairobi, mimi nikasema sio mimi lakini vile ilitokea hivyo, mtu mmoja akakuja akasema haya mambo twende Nairobi runingani tujue ukweli ni upi.”


Hata hivyo, baada ya kufika Nairobi, hakupelekwa runingani bali alijikuta amepelekwa kwa sosholaiti Manzi wa Kibera akatambulishwa kwa masuala ya kurekodi video.


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved