logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii stevo simple boy asema ni Kapera kwa sasa

Msanii wa Kenya Stephen Otieno Adera alimaarufu Stevo Simple boy alijiachillia aliposema kuwa kuwa yuko Single.

image
na Evans Omoto

Mastaa wako21 March 2025 - 16:39

Muhtasari


  • Alisema kuwa aliamua kuwa Kapera kutokana na sababu nyingi za Wasichana kumtenda kinyume na mapenzi yake.
  • Msanii Stevo  simple boy anajulikana kutokana na ubunifu wake wa  kuimba na kufanya mzaha kwa mashabiki wake ambao amekuwa akiwawacha vinywa wazi .

Msanii wa  Kenya Stephen Otieno  Adera alimaarufu  Stivo Simple boy alijiachillia aliposema kuwa  kuwa  yuko Single.

Alisema kuwa aliamua kuwa Kapera kutokana na sababu nyingi za Wasichana kumtenda kinyume na mapenzi yake.

Alipozungumza akiwa katika mahojiano mnamo Ijumaa ya Machi 21,2025, mzawa huyo wa Kibra aliweza kusema kuwa baada ya kupitia mapigo kadhaa kimapenzi ya kukataliwa na wasichana  aliowapenda aliamua kupiga hatua kimaisha na sasa hataki uhusiano.

Msanii Stevo  simple boy anajulikana kutokana na ubunifu wake wa  kuimba na kufanya mzaha kwa mashabiki wake ambao amekuwa akiwawacha vinywa wazi .

‘’Nilipigwa matukio sasa niko Single ,Wanadada walinikataa,sasa nikaamua mimi kama dragon,wacha tu niteme moto ‘’ Simple Boy alisema.

Maisha ya msanii stevo  simple boy yamechochea sana maisha ya wakenya akiwapendeza kama msanii mchangamfu na mcheshi mkuu.

Ipo siku aliwahi kumtambulisha mrembo kwa jina Pritty Vishy kama mrembo wake kabla ya wao kuachana kwa muda wa miezi michache.Hatimaye aliweza kumtambulisha msichana mwingine kwa jina GRACE kama mchumba wake lakini baadaye waliwachana tena.

Siku za hivi karibuni aliweza kupigwa na m shutuko baada ya kukumbuka kuhusu zaidi ya mahusiano na wapenzi wake wa zamani ambapo walimdanganya zaidi ya mara 10 Jambo lililomfanya abadili Mawazo na kusema atafikiria masuala ya mapenzi mwaka wa 2026.

Simple boy aliweza kusema kuwa kuna vitu ambavyo yeye huvichukia kama kukosa uaminifu katika uhusiano akikariri kuwa jambo hilo huweza kuchangia pakubwa kuporomoka kwa mapenzi.

Stevo alisema kuwa aliyekuwa mpenzi wake wa zamani  Grace aliweza kuzalishwa na mwanamume mwingine ilihali alikuwa na yeye bado katika mahusiano  jambo ambalo lilimkata maini sana na kujihisi mnyonge wa  mapenzi na mtoro kwa sasa.

Alisema kuwa hata baada ya Grace kujifungua mwana hakushughulika kutafuta babake mwana jambo ambalo lilimwacha akiwa amechanganyikiwa na kumwacha katika hali tete.

‘’Tulikuwa sawa hapo mbele tulikuwa tunaishi vizuri mke wangu alipokuwa karibu  kujifungua mtu alinipigia simu na akaninong’onezea kuwa alihitaji kuniambia jambo aliniambia kuwa ulikuwa wakati mwafaka wa mimi kuambiwa ukweli na kuniambia kuwa nisikasirike, aliniambia mtoto si wangu hilo jambo lilinicha na mawazo makubwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved