logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume mmoja akamatwa kwa kusababisha taharuki Lamu

Labda uliona video ya rais Kenyatta akionekana kushtuka wakati alipokuwa anapeana hotuba. Je, ni kipi kilichotokea?

image
na Radio Jambo

Habari21 May 2021 - 02:17

Muhtasari


•Kinyua alikamatwa baada ya kusababisha hali ya taharuki wakati rais anatoa hotuba

•Alisema kuwa alitaka kutoa lalamishi kuhusu ugavi wa kazi katika eneo hilo.

sherehe ya kuzindua bandari ya Lamu

Labda uliona video ya rais Kenyatta akionekana kushtuka wakati alipokuwa anapeana hotuba. Je, ni kipi kilichotokea?

Mwanaume mwenye umri wa wastani alikamatwa siku ya Alhamisi baada ya kujaribu kulamisha kumfikia rais Kenyatta alipokuwa anatoa hotuba katika sherehe ya kufungua bandari la Lamu.

James Kinyua Wamuchomba ambaye alidai kuwa alitaka kutoa lalamishi la kutoridhika na ugavi wa kazi kwa wenyeji wa eneo hilo anatarajiwa kufikishwa kotini siku ya Alhamisi.

Kinyua alikuwa baadhi ya waliokuwa wamealikwa. Aliwapita maafisa wa ulinzi ila akazuiwa akiwa amefika futi kidogo tu kumfikia rais wakati mmoja wa wasaidizi wake rais alipomuona na kujulisha maafisa.

Rais alimuona Kinyua akikaribia na kuonekana kushtuka ghafla ila maafisa walimshika alipokuwa anapiga kelele kwake rais.

Pole sana ni mtu tu na mambo yake” rais alisikika kusema baada ya tukio hilo.

Baada ya kukamatwa, Kinyua ambaye alikuwa ameshikilia kitambulisho chake tu alihojiwa ndipo akasema kuwa alitaka kutoa lalamishi kuhusu ugavi wa kazi katika eneo hilo.

“Alikuwa amejihami na kitambulisho tu kwa hivyo hatudhani alikuwa na lengo la chinichini. Hata hivyo, atashtakiwa pamoja na wengine kwa kusababisha usumbufu” Alisema afisa mmoja mkuu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved