logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kenya Kukumbatia RSF Kunaiweka Miongoni Mwa Mataifa Rogue – Serikali Ya Sudan

Mataifa kama vile Qatar, Misri, Saudi Arabia miongoni mwa mengine yamesimama kidete kutetea Sudani dhidi ya RSF na mikataba waliyotia saini Nairobi wiki juzi.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari03 March 2025 - 11:45

Muhtasari


  • Mataifa kama vile Qatar, Misri, Saudi Arabia miongoni mwa mengine yamesimama kidete kutetea Sudani dhidi ya RSF na mikataba waliyotia saini Nairobi wiki juzi.
  • Sudani iliendeleza Kauli za kutoa wito kwa jamii za kimataifa na haswa muungano wa bara la Afrika kuingilia kati 

Sudani yapongeza mataifa yaliyopinga shughuli za RSF Nairobi

SERIKALI ya Sudan imeendeleza mirindimo yake yak uikashifu serikali ya Kenya chini ya uongozi wake rais William Ruto baada ya kuwakubali wanamgambo wa kundi la RSF kukongamana Nairobi na kutia saini ya kuanzisha utawala mbadala jijini Khartoum.

Katika ujumbe wake mrefu kwenye X kupitia wizara ya masuala ya kigeni, Sudan ilipongeza hatua ya baadhi ya mataifa kutoka ukanda wa Mashariki ya Kati kupinga maelewano hayo yaliyotiwa saini jijini Nairobi siku chache zilizopita.

Mataifa kama vile Qatar, Misri, Saudi Arabia miongoni mwa mengine yamesimama kidete kutetea Sudani dhidi ya RSF na mikataba waliyotia saini Nairobi wiki juzi.

“Wizara ya Mambo ya Nje inafuata kwa shukrani na maslahi misimamo ya kimataifa iliyofuatana kukataa tishio kwa mamlaka na umoja wa Sudan na uhalali wa kitaifa uliopo humo kupitia jaribio la kuanzisha mamlaka kwa jina la wanamgambo wa Janjaweed na washirika wake, kuanzia Kenya, na chini ya usimamizi wa mfadhili wa kikanda wa wanamgambo.”

“Katika suala hili, Wizara ilipongeza misimamo mikali ya kanuni iliyoonyeshwa na Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Ufalme wa Saudi Arabia, Qatar, Kuwait, na nchi wanachama wa Baraza la Usalama la Afrika: Algeria, Somalia, na Sierra Leone, na misimamo ya nchi zingine wanachama wa Baraza: Urusi, Uchina, Amerika, Uingereza na Guyana, na taarifa iliyotolewa na Türkiye,” wizara hiyo ilisema.

Katika kile kilichoonekana kama ni kufuma zaidi mkuki kwenye moyo wa Kenya, Sudan iliikshifu Kenya ikisema kwamba kitendo chake kukubaslia RSF jukwaa la kufanya shughuli zake za kutafuta amani jijini Nairobi ni sawa na kuingia katika safu ya mataifa potovu duniani.

“Misimamo hii ya wazi inathibitisha kwamba tabia ya kutowajibika ya rais wa Kenya, kwa kukumbatia wanamgambo wa mauaji ya halaiki na kutaka kuhalalisha uhalifu wake ambao haujawahi kushuhudiwa, imeitenga nje na ndani, na kuiweka Kenya katika kundi la taifa potovu dhidi ya kanuni za kimataifa.”

Sudani iliendeleza Kauli za kutoa wito kwa jamii za kimataifa na haswa muungano wa bara la Afrika kuingilia kati ili kukomesha kile ambacho wanakiona kama ni ukiukaji mkubwa wa haki za kujitawala.

“Tunarudia wito wetu kwa wanachama wote wa jumuiya ya kimataifa na mashirika ya kikanda na kimataifa, hasa Umoja wa Afrika, kulaani tishio hili kubwa kwa amani na usalama wa kikanda na kuharibu sheria zilizowekwa za mfumo wa kimataifa,” ujumbe huo uliotolewa Jumatatu ulisema.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved