logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“7 ni namba takatifu!” Cherargei atetea hatua ya kutaka kuongezwa kwa muhula wa urais

“Jambo la kwanza unajua nambari 7 ni nambari takatifu kwetu sisi ambao ni Wakristo. Jambo la pili nimeshawaambia kwamba hili taifa limekuwa ni la kisiasa kwa muda wote."

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari23 April 2025 - 13:53

Muhtasari


  • Cherargei Alifichua kwamba kila mtu nchini Kenya amekuwa akiendesha siasa za kampeni tangu mwaka 2022 uchaguzi ulipokamilika.
  • Kulingana na seneta huyo, Kenya inastahili kuwa na sheria kama ya jirani Tanzania ambapo kuna sheria kali inayozuia kampeni za siasa nje ya kipindi cha mwaka au miezi 6 kabla ya uchaguzi mkuu.

Seneta Samson Cherargei

SENETA wa Nandi Samson Cherargei ametetea mswada wake unaolenga kuongezwa kwa muda wa muhula wa kuhudumu kwa rais kutoka kwa miaka 5 hadi 7.

Akizungumza katika mazungumzo na kituo kimoja cha redio humu nchini, mwandani huyo wa rais William Ruto alisema kwamba kando na kipindi hicho kumpa rais muda zaidi wa kufanya kazi na kutimiza ahadi zake kwa wapiga kura, pia nambari 7 kwa Wakristo ina umuhimu mkubwa.

“Jambo la kwanza unajua nambari 7 ni nambari takatifu kwetu sisi ambao ni Wakristo. Jambo la pili nimeshawaambia kwamba hili taifa limekuwa ni la kisiasa kwa muda wote, ni nadra sana kiongozi kupata muda wa kutosha wa kutekeleza majukumu yake,” Cherargei alieleza.

Cherargei Alifichua kwamba kila mtu nchini Kenya amekuwa akiendesha siasa za kampeni tangu mwaka 2022 uchaguzi ulipokamilika.

Kulingana na seneta huyo, Kenya inastahili kuwa na sheria kama ya jirani Tanzania ambapo kuna sheria kali inayozuia kampeni za siasa nje ya kipindi cha mwaka au miezi 6 kabla ya uchaguzi mkuu.

“Kuna rafiki yangu kutoka Tanzania alikuwa ananiambia katika sheria yao, ukiendesha kampeni nje ya mwaka mmoja au mwaka mmoja kabla ya uchaguzi unakamatwa na kushtakiwa. Lakini hapa Kenya watu wataanza kusema ni hujumu ya kidemokrasia,” Cherargei alisema.

Seneta huyo alitangaza kuwasilisha mswada huo mwaka jana ambapo analenga muhula wa kisiasa kuongezwa kutoka miaka 5 kama ilivyo kwa sasa chini ya katiba ya 2010, hadi miaka 7.

Hata hivyo, ni mswada ambao ulipokea maoni mengi ya kuupinga, japo seneta Cherargei bado anaonekana kuwa na azma ya kuufufua na kuuwasilisha bungeni.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved