logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Cherargei: Sio rahisi kuenda raundi 7 kama Raila AUC, tunajua watu wa dakika 1 sekunde 59

“Kwa hivyo tunamsherehekea na kukubali chenye alifanya, raundi 7 katika umri wake sio jambo rahisi kwenye kinyang’anyiro cha AUC,” aliongeza.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari21 February 2025 - 10:37

Muhtasari


  • Cherargei alisema kwamba Odinga katika umri wake – 80 – alijaribu sana kustahimili hadi raundi ya 6 ambapo aliamua 

Seneta Cherargei

SENETA wa Nandi, Samson Cherargei amewakashifu baadhi ya Wakenya wanaosherehekea kushindwa kwa Raila Odinga kwenye AUC.

Akizungumza katika kikao cha bunge la seneti Alhamisi, Cherargei alimpongeza Odinga kwa kustahimili kinyang’anyiro hicho kikali kuanzia kampeni hadi shughuli nzima ya upigani kura.

Cherargei alisema kwamba Odinga katika umri wake – 80 – alijaribu sana kustahimili hadi raundi ya 6 ambapo aliamua kujiondoa na kumuacha mgombea mwenza Mahmoud Youssouf kushinda katika raundi ya 7 kwa kura 33.

“Ningependa kushukuru mataifa 22 kutoka kwa umoja wa Afrika ambao walisimama na Raila Odinga kwa raundi 7. Raila Odinga alishinda raundi mbili na si rahisi kuenda raundi 7, tunajua watu ambao wanaenda kwa dakika 1 na sekunde 59 lakini katika umri wake, Baba Raila alijaribu kusimama kwa raundi 7 katika uchaguzi wa AUC,” Cherargei alisema.

“Kwa hivyo tunamsherehekea na kukubali chenye alifanya, raundi 7 katika umri wake sio jambo rahisi kwenye kinyang’anyiro cha AUC,” aliongeza.

×

Hata hivyo, Radio Jambo inaweza kuripoti kwamba Raila Odinga alijiondoa katika kinyang’anyiro hicho katika raundi ya 6 baada ya kupata kura 22 dhidi ya 26 za Youssouf kutoka Djibout.

Mgombea huyo wa Djibout alishinda katika raundi ya 7 ambayo alikuwa peke yake ambapo alihitajika kufikisha akidi hitajika ya kura 33 sawa na thuluthi mbili za kura.

Youssouf aliapishwa kama mwenyekiti mpya wa AUC ambaye alimrithi Moussa Faki.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved