logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Museveni Ampongeza Mahmoud Ali Youssouf Kufuatia Ushindi Wa Uchaguzi Wa AUC

Museveni ametuma salamu za pongezi kwa Mahmoud Ali Youssouf baada ya kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa AUC.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri18 February 2025 - 07:41

Muhtasari


  • Museveni pia alimpongeza Selma Malika Haddadi kwa kushinda nafasi ya Naibu Mwenyekiti wa Tume hiyo.
  • Museveni alisisitiza dhamira ya Uganda kushirikiana kwa karibu na Tume ya Umoja wa Afrika.

Mahmoud Youssouf amepongezwa na Rais Yoweri Museveni

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ametuma salamu za pongezi kwa Mahmoud Ali Youssouf baada ya kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC) katika Mkutano wa 38 wa Umoja wa Afrika.

Kupitia taarifa rasmi, Museveni pia alimpongeza Selma Malika Haddadi kwa kushinda nafasi ya Naibu Mwenyekiti wa Tume hiyo, akieleza kuwa Uganda inasalia kuwa mshirika mwaminifu wa Umoja wa Afrika katika juhudi za kutatua changamoto za bara hili na kutumia fursa zilizopo kwa manufaa ya wananchi wake.

"Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Uganda, na kwa niaba yangu binafsi, ninatoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Mahmoud Ali Youssouf na Selma Malika Haddadi kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti na Naibu Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika mtawalia katika Mkutano wa 38 wa AU," alisema Museveni.

Aidha, Rais Museveni alisisitiza dhamira ya Uganda kushirikiana kwa karibu na Tume ya Umoja wa Afrika ili kutafuta suluhisho kwa changamoto zinazolikumba bara la Afrika na kuboresha hali ya maisha ya raia wake.

Uchaguzi wa viongozi wa Tume ya Umoja wa Afrika huwa unafanyika kila baada ya miaka minne, na viongozi wapya wanatarajiwa kusimamia ajenda ya maendeleo ya bara hili, kushughulikia masuala ya usalama, diplomasia, na ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa wanachama wa AU.

Mahmoud Ali Youssouf, ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Djibouti, atachukua nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minne, akiongoza juhudi za kuimarisha mshikamano wa bara la Afrika katika nyanja mbalimbali.

Katika uchaguzi wa Jumamosi, Februari 16, Youssouf alishinda baada ya kupata kura zinazohitajika katika raundi ya saba, ambapo alikuwa mgombea pekee baada ya mgombea wa Kenya RailaOdinga kuondolewa katika raundi ya sita.

Richard Randriamandrato wa Madagascar aliondolewa mapema baada ya kushika mkia katika awamu ya kwanza, ya pili, ya tatu na ya nne na kuwaacha Raila na Youssof kumenyana.

Youssouf alitangazwa mshindi baada ya kupata kura 33 zilizohitajika katika raundi ya saba ya upigaji kura, ambayo alishinda peke yake.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved