logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jumuiya ya Wasioamini Mungu Wapongeza Marais wa Afrika Kutomchagua Raila AUC

Jumuiya hiyo inayoongozwa na Harrison Mumia ilisema kwamba kama kuna jambo la muhimu marais wa takriban mataifa 50 ya Afrika walifanya basi ni kutomchagua Raila Odinga.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani17 February 2025 - 13:15

Muhtasari


  • Raila Odinga alijiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho katika raundi ya 6 baada ya kujizolea kura 22 dhisdi ya 26 za Mahmoud Ali Youssouf kutoka Djibout.
  • Mgombea huyo wa Djibout alikwenda katika raundi ya 7 peke yake na kujizolea kura 33, ambazo ni thuluthi mbili iliyostahiki kupata mshindi.

Aliyekuwa mgombea wa wadhifa wa AUC, Raila Odinga

JUMUIYA ya watu wasioamini katika uwepo wa Mungu nchini Kenya wamepongeza viongozi wa mataifa ya Afrika kwa kutomchagua aliyekuwa mgombea wa uenyekiti wa AUC kutoka Kenya.

Wakizungumza kupitia chapisho kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii, Jumuiya hiyo inayoongozwa na Harrison Mumia ilisema kwamba kama kuna jambo la muhimu marais wa takriban mataifa 50 ya Afrika walifanya basi ni kutomchagua Raila Odinga.

Kwa mujibu wa jumuiya hiyo, Odinga alipaswa kufeli katika kinyang’anyiro hicho kwani alishachafua jina lake zuri alilolijenga kwa muda mrefu kuhusu kupigania haki za kibinadamu, pale alipoamua kujihusisha na serikali ya rais Ruto.

 Jumuiya ilisema kwamba serikali ya Kenya chini ya rais William Ruto imejizolea umaarufu katika mauaji na utekaji nyara, hivyo Raila kushirikiana nayo ni sawa na kupaka damu jina lake.

“Siku ya Jumamosi, Raila Odinga alishindwa vilivyo na mgombea wa Djibouti, Ali Youssouf, katika uchaguzi wa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika. Tunatoa pongezi zetu kwa Ali Youssouf na tunamtakia kila la kheri katika jukumu lake jipya.”

“Raila Odinga amewaangusha wananchi wa Kenya kwa kuachia wadhifa wake wa kiongozi wa upinzani, na kuunda muungano wa hila na Rais William Ruto. Inasikitisha kwamba, baada ya kujijengea taswira ya kuwa mtetezi wa haki za binadamu na uzingatiaji wa katiba, ameungana na serikali ambayo imekuwa maarufu kwa utekaji nyara, na utawala mbovu.”

“Kutokana na hali hiyo, tunaamini kuwa viongozi wa Afrika walifanya uamuzi wa busara kumnyima uenyekiti. Ni wakati wa Raila kujitenga na kuruhusu Wakenya kujiamulia mustakabali wao wenyewe,” jumuiya hiyo ilichapisha.

Raila Odinga alijiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho katika raundi ya 6 baada ya kujizolea kura 22 dhisdi ya 26 za Mahmoud Ali Youssouf kutoka Djibout.

Mgombea huyo wa Djibout alikwenda katika raundi ya 7 peke yake na kujizolea kura 33, ambazo ni thuluthi mbili iliyostahiki kupata mshindi.

Youssouf sasa ndiye mwenyekiti mpya wa tume ya Afrika ambaye amechukua uongozi kutoka kwa mwenyekiti anayeondoka, Moussa Faki.

 

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved