logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Farouk Kibet Atoa Onyo Kali Kwa Waandamanaji Kuhusu Uharibifu wa Mali

Maandamano hayo yalifuatia mauaji ya Ojwang, ambaye alifariki akiwa chini ya ulinzi wa polisi Jumapili.

image
na Tony Mballa

Habari22 June 2025 - 20:18

Muhtasari


  • Wakati wa maandamano hayo, mali iliharibiwa na magari mawili kuchomwa moto. Kibet alimtaka Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja kuchukua hatua na “kulinda” jiji dhidi ya uharibifu huo.
  • Akijibu wito huo, Gavana Sakaja alisema wale waliohusika na uharibifu wa mali ya umma jijini Nairobi wakati wa maandamano watakamatwa.

Farouk Kibet
Msaidizi wa Rais William Ruto, Farouk Kibet, amewaonya waandamanaji dhidi ya kuharibu mali ya umma na biashara za Wakenya wakati wa maandamano.

“Tumesema kuwa maandamano yasitumike kuharibu mali ya watu. Tunataka maandamano yawe ya amani, yaeleze maoni kwa mujibu wa sheria na si kisingizio cha kuharibu mali ya Wakenya,” alisema Kibet.

Kauli yake ilitolewa siku chache baada ya kumshutumu aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua kwa kuchochea maandamano ya hivi majuzi jijini Nairobi.

Farouk Kibet

Maandamano hayo, ambayo yalilenga kushinikiza hatua kuchukuliwa kuhusu mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang, yaliishia kuwa vurugu.

Polisi walitumia vitoa machozi na magari ya maji kuwatawanya waandamanaji hadi jioni.

Wakati wa maandamano hayo, mali iliharibiwa na magari mawili kuchomwa moto. Kibet alimtaka Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja kuchukua hatua na “kulinda” jiji dhidi ya uharibifu huo.

Akijibu wito huo, Gavana Sakaja alisema wale waliohusika na uharibifu wa mali ya umma jijini Nairobi wakati wa maandamano watakamatwa.

Farouk Kibet

Gavana huyo alisema kuwa uchunguzi wa kina utafanywa na wale watakaopatikana na hatia watakamatwa na kufikishwa mahakamani.

Sakaja alisisitiza kuwa katiba inaruhusu maandamano ya amani lakini si ya fujo, na kuwataka Wakenya, hususan wanasiasa, kuepuka siasa za mgawanyiko.

Maandamano hayo yalifuatia mauaji ya Ojwang, ambaye alifariki akiwa chini ya ulinzi wa polisi Jumapili.

Uchunguzi kuhusu kifo cha Ojwang katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Nairobi unaendelea, huku maafisa wa polisi waliokuwa kazini kituoni humo wakisimamishwa kazi.

Maafisa wa polisi, akiwemo OCS wa Kituo Kikuu cha Polisi Samson Talaam na James Mukhwana, wamekamatwa.

Mamlaka Huru ya Uangalizi wa Polisi (IPOA) inaendelea na uchunguzi kuhusu suala hilo.

Farouk Kibet

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved