Jackton Odhiambo, mshukiwa mkuu katika mauaji ya mwanaharakati wa LGBTQ Edwin Kiprotich Kiptoo maarufu kama Chilloba anatarajia kusikiliza hukumu dhidi yake mnamo Disemba 16, 2024 baada ya mahakama kuu ya Eldoret kumpata na hatia katika kesi iliyosikilizwa Jumatano Disemba 4.
Hukumu kwa Jackton inajiri takribani miaka miwili tangu kuripotiwa kwa kuawa kwa ‘Chiloba’ katika eneo la Kimumu, jijini Eldoret mnamo Disemba 31, 2022.