logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshukiwa wa mauaji ya ‘Chiloba’ kuhukumiwa Disemba 16 na mahakama ya Eldoret

Mahakama kuu ya Eldoret ilimpata Jackton na hatia ya kumwuua 'Chiloba' mnamo mwaka wa 2022

image
na Brandon Asiema

Mahakama05 December 2024 - 10:14

Muhtasari


  • Hukumu kwa Jackton inajiri takribani miaka miwili tangu kuripotiwa kwa kuawa kwa ‘Chiloba’ katika eneo la Kimumu, jijini Eldoret mnamo Disemba 31, 2022.


Jackton Odhiambo, mshukiwa mkuu katika mauaji ya mwanaharakati wa LGBTQ Edwin Kiprotich Kiptoo maarufu kama Chilloba anatarajia kusikiliza hukumu dhidi yake mnamo Disemba 16, 2024  baada ya mahakama kuu ya Eldoret kumpata na hatia katika kesi iliyosikilizwa Jumatano Disemba 4.

Hukumu kwa Jackton inajiri takribani miaka miwili tangu kuripotiwa kwa kuawa kwa ‘Chiloba’ katika eneo la Kimumu, jijini Eldoret mnamo Disemba 31, 2022.