logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KEMSA yaahidi kuimarisha usambazaji vifaa vya matibabu katika kaunti

Alisema halmashauri ya KEMSA imetoa dawa za thamani ya shilingi bilioni 27 kote nchini

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 August 2022 - 19:31

Muhtasari


  • Ramadhani amesema halmashauri hiyo inalenga kukusanya angalau shilingi milioni 500 kila mwezi kutoka serikali za kaunti ili kuboresha utoaji huduma

Halmashauri ya usambazaji dawa hapa nchini (KEMSA) imeahidi kusaidia ajenda ya kuhimiza afya njema katika kiwango cha kaunti ya magavana wapya kama shemu ya mkakati wa mageuzi wa halmashauri hiyo.

Akiwa na wa gavana mteule wa kaunti ya Garissa Nathif Jama, siku ya Alhamisi afisini mwake , afisa mkuu mtendaji wa halmashauri ya KEMSA Terry Ramadhani, alisema serikali za kaunti ni wateja wa halmashauri hiyo na kwamba halmashauri hiyo inafanya kila juhudi katika kuhakikisha wanatimiza awamu ya mwisho ya mahitaji ya usambazaji dawa.

Alisema halmashauri ya KEMSA imetoa dawa za thamani ya shilingi bilioni 27 kote nchini wakati wa mwaka uliopita wa kifedha.

Ramadhani amesema halmashauri hiyo inalenga kukusanya angalau shilingi milioni 500 kila mwezi kutoka serikali za kaunti ili kuboresha utoaji huduma.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved