logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wikendi ya unyevunyevu maeneo mengi yakitabiriwa kushuhudia mvua nyingi

Wikendi ya unyevunyevu maeneo mengi yakitabiriwa kushuhudia mvua nyingi

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri28 March 2025 - 16:51

Muhtasari


  • Sehemu ambazo zinatarajia mvua kubwa ni pamoja na Nyanda za Juu Magharibi mwa Bonde la Ufa, Bonde la Ziwa Victoria.
..
Mvua inatarajiwa kuendelea kunyeshakatika sehemu kadhaa za nchi.

 Matukio ya mvua kubwa ya pekee yanaweza kutokea katika baadhi ya maeneo ya Nyanda za Juu Mashariki na Magharibi mwa Bonde la Ufa, Bonde la Ziwa Victoria.

Sehemu zingine ambazo zinatarajiwa kupokea mvua ni Bonde la Ufa, nyanda za chini za Kusini-mashariki, Pwani, Kaskazini-mashariki na Kaskazini-magharibi mwa Kenya

Sehemu ambazo zinatarajia mvua kubwa ni pamoja na Nyanda za Juu Magharibi mwa Bonde la Ufa, Bonde la Ziwa Victoria.

Maeneo haya yanajumuisha kaunti zifuatazo(Siaya, Kisumu,Homabay, Migori, Kisii, Nyamira,Trans Nzoia, Baringo, Uasin Gishu,Elgeyo-Marakwet, Nandi, NakuruNarok, Kericho, Bomet, KakamegaVihiga, BungomaBusia na Pokot.

Kaskazini-magharibi (Turkana na Samburu] zitapokea mvua chache siku ya Jumamosi. Nyakati za asubuhi na usiku kutakua na kijibaridi kikali huku majira ya mchana yakishuhudia jua.

Kaskazini-mashariki (Marsabit,Mandera, Wajir, Garissa na Isiolo] Kaunti hizi zitapokea mvua ya mfululizo kwa siku tatu zijazo kuanza Ijumaa. Baadhi ya sehemu za kaunti hizo zitafunikwa na wingu zito na jua kwa asilimia chache mno.

Nyanda za chini za kusini-mashariki (Kitui, Makueni, Machakos, Kajiado na  Kaunti za Taita Taveta na vile vile sehemu za bara za Kaunti ya Tana River.) 

Sehemu hizi zitapokea mvua karibu maeneo yote siku ya Ijumaa, Jumamosi na Jumapili. Baadhi ya sehemu hizo mvua itaandamana na ngurumo za radi.

Maeneo ya Pwani (Mombasa, Kilifi, Lamu na Kaunti za Kwale pamoja na pwani sehemu za Mto Tana.) zitapokea mvua chache. Mvua ya rasharasha itashudiwa kwenye baadhi ya sehemu siku ya Jumamosi na Jumapili. Sehemu nyingi za maeneo hayo zitapokea joto la kadri kati ya nyusi 23'C - 36' C.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved