logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kevin De Bruyne ametangaza kuondoka Manchester City mwishoni mwa msimu

Mbelgiji huyo amecheza mechi 280 za Premier League kwa kikosi cha Pep Guardiola, akifunga mabao 70 na kutoa asisti 118 kwenye mashindano hayo

image
na MOSES SAGWEjournalist

Michezo04 April 2025 - 16:12

Muhtasari


  • Mbelgiji huyo amecheza mechi 280 za Premier League kwa kikosi cha Pep Guardiola, akifunga mabao 70 na kutoa asisti 118 kwenye mashindano hayo.
  • "Tupende tusipende, ni wakati wa kusema kwaheri. Suri, Rome, Mason, Michèle, na mimi tunashukuru sana kwa nini eneo hili limemaanisha kwa familia yetu."

Kevin De Bruyne, mchezaji wa Manchester City atangaza kuondoka mwisho wa msimu 2024/25//INSTAGRAM

KIUNGO wa kati wa Manchester City Kevin De Bruyne ametangaza kuwa ataondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu kufuatia miaka 10 ya kubebea mataji kwenye Uwanja wa Etihad.

De Bruyne, bingwa mara sita wa Premier League akiwa na Man City, alitangaza uamuzi wake huo katika taarifa ya hisia kwenye mitandao ya kijamii siku ya Ijumaa.

Mbelgiji huyo amecheza mechi 280 za Premier League kwa kikosi cha Pep Guardiola, akifunga mabao 70 na kutoa asisti 118 kwenye mashindano hayo, jumla ya mabao hayo ikiwa ya pili baada ya rekodi ya muda wote ya Ryan Giggs ya 162.

Katika taarifa yake De Bruyne alisema: "Wapendwa wa Manchester, ukiona hili, labda unatambua wapi hii inaelekea. Kwa hivyo nitaingia moja kwa moja na kuwafahamisha kuwa hii itakuwa miezi yangu ya mwisho kama mchezaji wa Manchester City.”

"Kandanda iliniongoza kwa nyinyi nyote-na kwa jiji hili. Kukimbiza ndoto yangu, bila kujua kipindi hiki kungebadilisha maisha yangu. Jiji hili. Klabu hii. Watu hawa ... walinipa KILA KITU. Sikuwa na chaguo ila kurudisha KILA KITU! Na tafakari hili, tulishinda KILA KITU.”

"Tupende tusipende, ni wakati wa kusema kwaheri. Suri, Rome, Mason, Michèle, na mimi tunashukuru sana kwa nini eneo hili limemaanisha kwa familia yetu. 'Manchester' itakuwa kwenye hati za kusafiria za watoto wetu milele - na muhimu zaidi, katika kila moja ya mioyo yetu. Hii itakuwa NYUMBANI kwetu daima.”

"Hatuwezi kuwashukuru City, klabu, wafanyakazi, wachezaji wenzetu, marafiki na familia vya kutosha kwa safari hii ya miaka 10. Kila hadithi inaisha, lakini hii imekuwa sura bora zaidi. Hebu tufurahie nyakati hizi za mwisho pamoja! Nawapenda sana, KDB,” barua yake ilisomeka kwa ukamilifu.

Mbali na mataji yake sita ya Ligi Kuu ya England, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 alitawazwa Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Uingereza mara mbili, 2019/20 na 2021/22, na pia alishinda tuzo ya Playmaker wa assists nyingi zaidi katika msimu mara tatu, 2017/18, 2019/20 na 2022/23.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved