
Reuben Wanyonyi mwenye umri wa miaka 27 kutoka Bungoma alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na
shemeji yake Shadrack Simiyu (25) ambaye alikosana naye takriban miaka miwili
iliyopita.
Reuben alisema uhusiano wake na Shadrack uliharibika mwaka wa 2023 wakati aliacha kazi ambayo shemejiye huyo alikuwa amempea.
Alieleza kwamba jambo hilo limeleta misukasuko kwenye ndoa ya dadake.
“Ilikuwa 2023, shemeji yangu alikuwa anafuga kuku. Aliniajiri akasema nifanye kazi. Nikafanya kwa miezi tatu, hakunipea pesa. Nikaamua kuachana na kazi. Shemeji akaona vibaya akaanza kuniuliza mbona naacha kazi. Shemeji alisema mradi tu nipate chakula pesa nyingine atanipea. Naona ni kama alitaka mradi nikule, nilale na nimfanyie kazi. Mimi niliona ni ngumu,” Reuben alisimulia.
Reuben alisema shemejiye amekuwa akitishia dadake kwamba atamfukuza tangu alipoacha kazi hiyo.
“Wakati nilienda akaona ni kama dadangu alifanya niache kazi. Kuanzia hapo hatuongei, dadangu ananipigia simu ananiambia shemeji anampeleka vibaya anasema atamfukuza kwa sababu niliacha mali yake na ni mimi tu alikuwa naye naweza kumfanyia kazi,” alisema.
“Nilitaka kumwambia niliacha kazi kwa sababu niko na mahitaji mengi. Niko na mtoto mdogo. Nataka ajue nilienda kwa sababu kazi haikuwa inanipea pesa ya kutosha na nisifanye aachane na dadangu, nisije nikawa wa kuwatenganisha,” aliongeza.
Shadrack alipopigiwa simu aliweka wazi kwamba Reuben alimkosea sana.
“Hiyo maneno niliachana nayo hivyo. Alinikosea sana nikaachana
na hiyo maneno kabisa,” alisema kabla ya kukata simu.
Reuben alisema, “Shida yangu ni kuwa dadangu anasema anamvuruga, anamwambia ataenda kama kakake aliacha vitu zake akaenda. Dadangu akifanya kitu anaweka hapo jina langu. Dadangu amejaribu kuripoti kwa wazazi lakini shemeji anapatia baba kakitu mzee ananyamaza tu.”
Alipopewa nafasi ya kumwambia shemejiye ujumbe wa mwisho, Shadrack alimwambia, “Shadrack, kazi sikuacha kwa ubaya kwa sababu ile pesa ulisema utanipea sikuacha kwa ubaya. Isiwe ni mimi nitafanya mkosane. Kama nilikukoea naomba unisamehe na muendelee na maisha yenu vizuri.”
Je, una maoni ama ushauri gani kuhusu Patanisho ya leo?