logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Msichana wa Pwani akatiza mawasiliano na mpenziwe ghafla baada ya kutembelea kwao Siaya

Tony alisema uhusiano wake wa miaka miwili ulianza kuyumba baada ya mpenziwe kurudi kwao Mombasa.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho03 March 2025 - 08:38

Muhtasari


  • "Mambo imekuja ikabadilika. Alirudi Mombasa hivi majuzi. Nimekuwa nampigia simu hapokei," Tony alisema.
  • Tony alifichua kwamba mwanadada huyo tayari amemblock kwenye laini zake zote.

Warangazaji

Jamaa aliyejitambulisha kama Tony Omondi (25) kutoka Siaya alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mpenzi wake Faith Naunga (26) ambaye alikosana naye hivi majuzi.

Tony alisema uhusiano wake wa miaka miwili ulianza kuyumba baada ya mpenziwe kurudi kwao jijini Mombasa.

“Tumekuwa kwa mahusiano miaka miwili. Tulikuwa tukichumbiana tukipanga kuoana. Mambo imekuja ikabadilika. Alirudi Mombasa hivi majuzi. Nimekuwa nampigia simu hapokei. Amekuwa akijua tunapanga kuoana,” Tony alisema.

Aliongeza, “Naomba aniambie msimamo wake ili nijue hatua ya kuchukua.”

Faith alipigiwa simu lakini akakata pindi baada ya kufahamishwa anatafutwa na Tony.

Tony alisema kwamba hatua ya mpenziwe huyo ni thibitisho tosha kwamba hamtaki.

“Nimekubali matokeo juu siwezi lazimisha. Kuanzia mwanzo tulikuwa tunapendana. Nilikuwa namtumia tiketi ya kutoka Mombasa kuja Mombasa, na akakuja. Ni msichana wa Kipwani. Nilikuwa tu hali ya kikazi huko Mombasa tulipojuana lakini kazi ikaja kuisha. Huwa nang’ang’ana kimwanaume ilimradi tu apate chenye anataka,” Tony alisema.

Alifichua kwamba mwanadada huyo tayari amemblock kwenye laini zake zote.

“Nimeridhika. Hiyo ni dhibitisho tosha kwamba hataki mambo na mimi. Namba zangu zote ameziblock. Juzi nilimpigia na namba hajui, kuskia sauti yangu akakata. Hakuna kitu nilimfanyia. Nilikuwa tayari kumuomba msamaha. Kama imekataa, ibaki hivyo,” alisema.

Je, una ushauri ama maoni gani kuhus Patanisho ya leo?

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved