logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa amlalamikia mkewe kwa kutokula ugali, nyama, omena alizompikia baada ya kumkosea

Wanjala alisema ndoa yake ya miaka miwili iliharibika baada ya yeye kutumia pesa kwa njia ambayo haikumfurahisha mkewe.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho05 March 2025 - 06:13

Muhtasari


  • Wanjala alisema tangu wakosane hawajakuwa wakizungumza vizuri kwa nyumba na amekuwa akipika chakula na mkewe hali.
  • “Tulikuwa tumechukua pesa kujenga nyumba jioni. Badala hiyo pesa apate tulipe nusu, yeye alilipa simu,” Jackline alilalamika.

Gidi na Ghost

Danstan Wanjala (24) kutoka Kitengela alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mke wake Jackline Kasinda (23) ambaye alikosana naye hivi majuzi.

Wanjala alisema ndoa yake ya miaka miwili iliharibika baada ya yeye kutumia pesa kwa njia ambayo haikumfurahisha mkewe.

Alisema tangu wakati huo hawajakuwa wakizungumza vizuri kwa nyumba na amekuwa akipika chakula na mkewe hali.

“Juzi nilipata pesa kidogo nikaona nilipe simu yangu juu ni ya M-kopa. Yeye alikuwa amepanga kufanyia pesa kitu ingine. Vile alikuja jioni akajua vile nimetumia pesa. Akaniuliza kwa nini nililipa simu na alikuwa amepangia hiyo pesa. Mimi sikujua kuna matumizi mengi alikuwa anataka kufanyia pesa,” Wanjala alisema.

Aliongeza, “Hivyo ndo alinyamaza.Sasa tukiwa kwa nyumba hatuzungumzi. Hapo awali akienda kazi alikuwa ananiambia goodbye bebi, sasa haniambii. Mimi ndiye huwa napika kila siku juu huwa anatoka kazi kuchelewa. Tangu tukasirikiane, sio rahisi akule lakini akipata anakula. Jana nilipika ugali na omena, nikangoja aje tule. Alipofika akasema ameshiba.”

Jackline alipopigiwa simu, alisisitiza kwamba alikasirika kuhusu maamuzi ya kifedha ya mumewe.

“Tulikuwa tumechukua pesa kujenga nyumba jioni. Badala hiyo pesa apate tulipe nusu, yeye alilipa simu,” Jackline alilalamika.

Wanjala alijitetea kwa kusema alihofia simu yake kuzimwa.

Jackline alimwambia, “Hapo ulifanya makossa ungekuja uniambie umepata pesa fulani tupange vile tutatumia. Hiyo pesa ungepeana kwa loan.”

Wanjala alilalamika kuhusu jinsi amekuwa akijaribu kumfurahisha mkewe na haskii.

“Nimepika ugali na kuku ili ufurahie, lakini hukufurahia. Jana nikapika ugali na omena ndo ukuje ukule, na hukula.. Jioni nikienda kwa nyumba tutaongea tujue vile tutalipa hiyo pesa. Nisamehe kama nimekosea. Fanya moyo wako uwe mwepesi ndiyo unisamehe. Sitarudia,” alisema.

Jackline alikubali kumsamehe na kumhakikishia kuhusu upendo wake kwake.

“Mimi sina ubaya na wewe. Nampenda, tutarudi kukaa vile tulikuwa tunakaa hapo nyuma lakini asirudie hiyo makosa,” alisema.

Je, una  ushauri ama maoni gani kuhusu Patanisho ya leo?



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved