logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Siko sure kama huyo ndiye baba mtoto!" Mwanadada atofautiana vikali na aliyekuwa mumewe

Stella alisema kwamba amelea mtoto pekee yake n ahata akaibua utata kwamba hana uhakika kuhusu baba mtoto.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho10 March 2025 - 09:20

Muhtasari


  • Ouma alisema uhusiano wake na Stella uliharibika mwaka wa 2017 wakati mzazi huyo mwenzake alipoenda kusoma katika chuo cha KMTC Kisumu.
  • “Kunipata lazima akuwe na connections. Sijaongea na Ouma tangu 2013. Yeye amove on," Stella alisema.

Watangazaji

Wycliffe Ouma (34) kutoka Kisumu alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na aliyekuwa mke wake Stella Ayitso (32) ambaye alikosana naye takriban miaka saba iliyopita.

Ouma alisema uhusiano wake na Stella uliharibika mwaka wa 2017 wakati mzazi huyo mwenzake alipoenda kusoma katika chuo cha KMTC Kisumu.

Alisema mkewe alianza kubadilika baada ya kuwa shule kwa miezi sita, kabla ya kukatiza uhusiano naye kabisa baada ya muda.

“Tulipatana na yeye 2012. Alikuwa form 4. Alikuwa afanye mtihani mwaka huo. Tuliongea alirudi baada ya mwezi moja. Aliporudi kwao, aliniambia ako na mimba. Vile alimaliza mtihani wa kidato cha nne aliogopa kukaa nyumbani. Aliongea na rafiki yake, wakakuja tukakaa na wao,” Ouma alisimulia.

“Tulikaa mpaka mtoto akafika umri wa kuenda shule. Baada ya mtoto kufikisha miaka mitatu alirudi shule kusoma, alienda KMTC Kisumu. Mimi ndiye nilikuwa nampa nauli anaenda shule. Baada ya kusoma miezi kama sita, alianza kurudia nyumbani baada ya wiki tatu, akaanza kurudi baada ya mwezi mmoja. Hivyo ndivyo alienda kabisa. Wakati huo mtoto alikuwa na mamangu. Alifanya mpango akaenda akachukua mtoto,” aliongeza.

Ouma alidai kwamba dadake Stella alimwambia kuwa mkewe huyo wa zamani tayari ameolewa na Mnigeria ambaye anaishi naye Nairobi.

“Mimi ni Mjaluo na siwezi kuacha mtoto nje. Hiyo ndiyo inaniuma. Ata mimi nilishaoa. Niko na mtoto wa mwaka moja. Stella ashamove on, mimi nataka tu kujua msimamo wa mtoto,” alisema.

Stella alipopigiwa simu, aliweka wazi kwamba tayari amesonga mbele na maisha yake na mtoto anaendelea vyema.

Alisema kwamba amelea mtoto pekee yake n ahata akaibua utata kwamba hana uhakika kuhusu baba mtoto.

“Mimi nilishamove on kitambo sana. Mtoto ako sawa. Hafai kunisumbua kabisa. Nilienda shule, sikumuacha. Alinichukua illegally, mimi nikarudi chuo, nikaendelea. Ilikuwa 2012 baada ya kumaliza shule ya upili, nikazaa nikarudi shule. Mtoto ako na baba mwingine na ako sawa. Mtoto sasa ako na utambulisho mwingine,” Stella alisema.

“Mimi nimelea mtoto pekee yangu. Wewe unajua anakaa aje? Kwetu walikuwa strict sana, nikaamua nyumbani nikawaambia nataka kusoma. Nikapeleka mtoto kwao, wakasema hizo bajeti za shule ni mingi wakashindwa kugharamia. Siko sure kama huyo ndiye babake. Nitakubali afanye DNA. Huyo mtoto ananifanana, na ni kijana,” aliongeza.

Ouma aliweka wazi kwamba ataelekea kortini ili kupata haki ya kumuona mtoto wake. Pia alisema kwamba watafanya DNA.

Stella aliibua madai kwamba hajazungumza na Ouma kwa zaidi ya mwongo  mmoja. Pia aliweka wazi kwamba sio rahisi kumpata.

“Kunipata lazima akuwe na connections. Sijaongea na Ouma tangu 2013. Yeye amove on. Amekuwa akinitafuta, mimi sishiki simu zake. Kama atanitafuta ni sawa, lakini saai mtoto ako kwa mikono yangu. Asinitafute ashachoma kabisa,” alisema.

Ouma alimuomba mkewe huyo wa zamani awe anashika simu kila anapompigia.

Je, una ushauri ama maoni gani kuhusu Patanisho ya leo?


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved