logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Simjui !" Jamaa amkana waziwazi mpenzi wake mwenye ujauzito wa miezi 7

Omondi alipopigiwa simu alidai kwamba hamtambui Caroline kisha kukata simu mara moja.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho09 April 2025 - 09:05

Muhtasari


  • Caroline alisema uhusiano wake na Omondi wa miaka 8 uliharibika Desemba wakati mpenzi alikatiza mawasiliano naye baada ya kuenda nyumbani.
  • Caroline alifichua kwamba mara ya mwisho ambapo alipokea ujumbe kutoka kwa mpenziwe ilikuwa Desemba 18.

caption

Mwanadada aliyejitambulisha kama Caroline Kathambi mwenye umri wa miaka 29 kutoka Kayole alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mchumba wake Felix Omondi (40) ambaye alikosana naye miezi kadhaa iliyopita..

Caroline alisema uhusiano wake na Omondi wa miaka 8 uliharibika Desemba mwaka jana wakati mpenzi alikatiza mawasiliano naye baada ya kuenda nyumbani.

Aidha, alifichua kwamba kwa sasa ana ujauzito wa miezi 7, ambao alipata kinyume na matakwa ya mpenziwe.

“Mwezi Desemba mwaka jana nilikuwa naenda nyumbani Christmas. Wakati huo nilikuwa mgonjwa, na nilikuwa na mimba. Nikamwambia niende nikae nyumbani juu mambo si mazuri sana. Hatukuwa tunaishi na yeye awali. Tukaongea akasema ni sawa niende juu maisha Nairobi sio mazuri. Mimi nikaenda tu, ata hakunipea nauli. Nilienda nyumbani nikakaa,” Caroline alisimulia.

Caroline alifichua kwamba mara ya mwisho ambapo alipokea ujumbe kutoka kwa mpenziwe ilikuwa Desemba 18.

 “Nikimtext ama kumpigia simu hashiki. Hivyo tu ndio alininyamazia imagine. Sasa tarehe 16 kumbe ilikuwa siku ya mwisho aliniongelesha. Aliniandikia tu meseji akaniambia maisha Nairobi ni ngumu sana ata hana chochote,” aliongeza.

“ Bado sijajifungia, niko na mimba ya miezi saba sasa. Meseji huwa anapokea vizuri lakini hawezi jibu, nikimpigia ni kama ameniblock. Tumekuwa na yeye miaka nane, lakini hatukuwa tunaishi pamoja. Tulikuwa tunapenda juu alikuwa anakuja kuniona ata kama sio kila siku,” alisema.

Omondi alipopigiwa simu alidai kwamba hamtambui Caroline kisha kukata simu mara moja.

“Simjui mtu kama huyo tafadhali,” alisema.

Caroline alisema, “Simu zangu huwa hashiki. Ata meseji huwa hajibu. Alikuwa ameniambia hataki mimba. Labda shida ni hiyo. Mimi sijui nilishika mimba aje, ata mimi mwenyewe sikuwa nataka pia na sikuwa natarajia… Ni sawa tu hakuna njia nyingine. Nitakubali tu.”


Katika maneno yake ya mwisho kwa mpenziwe, Caroline alisema, “Felix naomba tu kama nimewahi kukusea unisamehe. Tafadhali tu kwa ajili ya huyu mtoto, unisaidie vile tutalea.”


Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved